Tuesday, February 9, 2010

NI SIKU IPI ILIKUUMIZA SANA MAISHANI MWAKO NA USINGEPENDA ITOKEE TENA????



MM SITASAHAU SIKU NESI ALIVYOMVIRIGA SHUKA MWANANGU WA KIUME AKIDHANI  AMEKUFA! KUMBE NI MZIMA!

MIMI  KWA UPANDE WANGU, siku ambayo sitaisahau maishani mwangu ni siku ambayo nesi alifikiri mwanangu amekufa na kumviriga katika shuka ili mchukuwa mait akija amchukuwe na yeye, aisee, siku ile hadi leo nikikumbuka huwa moyo unaniuma sana, nina watoto wangu wawili (TWINS) baada ya kujifungua niliruhusiwa kwenda nyumbani, nikaka wiki moja waototo wakaanza kuumwa nikawarudisha tena hospitali,(Muhimbili)  nikalazwa, basi kama ilivyokawaida mtoto mchanga akilazwa, wanalazwa kwenye ward yao nyie wazazi kazi yenu kwenda kunyonyesha tu! kila baada ya masaa matatu,

basi mwenyewe ndio wanangu wa kwanza hao tena mapacha, wa kike na wakiume, niliwapenda kama roho yangu, baada ya siku mbili kupita mwanangu wa kiume hali yake ilikuwa mbaya zaidi, akawekewa oxgen kwa ajili ya kumsadia kupumua, nilipoendakunyonyesha mida ya saa sita, hali yake haikuwa shwari kabisa, lakini huwa namwamini Mungu sana, nilikazana kuomba na kumwambia Mungu, niachie watoto wangu? lakini kama ni mapenzi yako basi na yatimizwe ! Ilifika kipindi nikawa nalia tu! 

Baada ya kwenda saa tisa tena kunyonyesha, sikumkuta mwanangu kitandani, nilimkuta mmoja tu! yule wa kike ambae nae alikuwa anaumwa, nikauliza wenzangu walioanza kuingia, jamani mwanangu yuko wapi? mmoja wao akanionyesha chini ya kitanda, na kusema bahati mbaya!, amekufa!  nilijikuta naishiwa nguvu na kuanguka chini huku nikilia sana na kwa sauti, basi wakaja wakanishika wakati wananitoa nje tuko mlangoni tukakutana na Dr. mmoja mlangoni, akauliza nini? na kwanini kama mtoto wake amefariki mmemruhusu kuingia huku? wakamwambia kuwa nina watoto wawili, hivyo niliruhusiwa kuingia ili nikanyonyeshe aliebaki

Mungu wa ajabu jamani, yule Dr. akaingia hadi ndani na kuuliza yuko wapi aliekufa, wakamwonyesha, akamfungua shuka, kukuta katoto kanahema ila kwa mbaaaali kabisa, alicho kifanya na sitasahau alisema hivi
FUTA MACHOZI YAKO! MUOMBE MUNGU MTOTO WAKO NI MZIMA NGOJA NIMSHUHURIKIE, NISIKUSIKIE UNALIA HATA KIDOGO!, nilipata nguvu za ghafla nikasimama nikamfata Dk. nikamuangalia alichokuwa akifanya, alimuingiza mtoto puani mpira, akawa anamjaza hewa, gafla tumbo la mtoto likawa kubwaaaaa, akatoa ule mpira akamchukuwa mtoto wangu hadi kitandani akamuewekea mpira mwingine mdogo wa oxgen na kuniambia kila nikiingia kunyonyesha nihakikishe mpira uko pale pale puani, kisha akamuita yule nesi aliekuwa zamu na kuondoka nae, ambae sielewi ni action gani ilichukukuliwa juu yake, maana hadi naruhusiwa hospitali sikumtia machoni tena,

Kumbe pale alipokuwa amewekwa mwanzoni ni kwamba alikuwa akisubiriwa mchukuwa maiti aje azikusanye, hatimaye mwanangu aakawa mzima, huwa nikimuangalia simmmalizi, Mungu alinitetea sana, na nilisimama katika imani tu! nilikaa muhimbili  mwezi mzima, lakini MUNGU WANGU NI MWAMINIFU hadi leo wanangu ni wazima kabisa, na nikiwaangali tu! huwa nafurahi sana, nawapenda mno,  na siku ileile nilimsamehe yule nesi,

NA HAWA NDIO TWINS WANGU, TRACY & TYMON  ni wazima kabisa
na hapo walipiga mwaka jana mwezi wa tatu walikuwa wanatimiza miaka mitatu,
wamesheaanza kusoma, basi huyo mtoto wa kiume nikimuangalia, Mh! namshukuru Mungu tu!


16 comments:

  1. aisee pole sana dada!
    story yako imenisikitisha sana, pole sana mdogo wangu, kumbe watoto wengi wanakufa kizembe sana, MUNGU NA AKUKUZIE WATOTO WAKO VIOLET

    ReplyDelete
  2. Nakusalimu katika Jina La yesu,

    Pole kwa sana dada na hongera kwa kumngangania Mungu, wanawake kama wewe ndio wanaohitajika katika kungangania.

    Mi ushauri wangu ni kumfanyia maombi ya ukombozi mwanao kwa ile roho ya mauti iliyotaka kumchukua.

    Kwa kweli kama sio huyu Mungu, sijui nisemeje.Hongera kwa ushindi. Kumbuka kumsamehe na usahau maana Mungu anasema anasamehe na anasahau. jitahidi kumwomba Mungu akupe neema ya kusahau kibinadamu hutaweza.

    ReplyDelete
  3. Mh! Pole dada Violet, nimeumia as if ndo hicho kitu kinatendeka muda huu, kweli mungu ni mwema na tumshukuru kwa kila jambo. Endelea kuomba na kushukuru nami nakuombea mungu akukuzie katika maadili mema.

    Binafsi sitasahau siku ambayo nilifiwa na baba yangu kifo cha ghafla, bila hata ya kuumwa wala nini. 02/04/2009, mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, amina. Nilimpenda sana baba yangu lakini Mungu alimpenda zaidi.

    Amanda

    ReplyDelete
  4. MOJA KATI YA MADA ULIZOPOST NI ILE YA KUSEMA JE MACHOZI NI SULUHISHO LA MATATIZO YA MWANAMKE? Mimi nilipinga, nikasema sio suluhisho
    LAKINI KWA HII STORY YAKO YA LEO, Nimekubali kwamba machozi yanaweza kusaidia sana, JIULIZE
    1. USINGELIA KWA SAUTI DOKTA ANGEKUJA KUMUONA MWANAO?
    2. MCHUKUWA MAITI ANGEKUMCHUKUA MTOTO ANGEENDA KUFIA WAPI KAMA SI MOCHWARI?
    3. ULIKUMBUKA KUMSHUKURU MUNGU??
    4. NASISITIZA KUMSAMEHE HUYO NESI
    nimejikuta natoa machozi Violet, watoto wako wazuri sana, wamekuwa, nimejaribu kumuangalia huyo TRACY, it means kwamba sasa hivi angekuwa peke yake, na hy angekufa pasipo mpango wa Mungu, KUMBE SOMETYMES KULIA KUNASAIDIA SANA
    VIOLET NIMEHUZUNISHWA SANA, SIKUJUI NA WALA HUNIJUI, ILA NINACHOKUOMBA TU! KAMA HUKUMSHUKURU MUNGU JUU YA HILI, NENDA KASHUKURU HARAKA SANA! maana bila Mungu usingekuwa na huyo mtoto, kamrudishie shukrani Mungu,
    kweli hata kama mimi nisingeisahau hiyo siku

    NIMEUMIA SANA.

    ReplyDelete
  5. nimelia sana Violet kutokana na hii story yako,
    nimefikiria mbali sana, nimefikiria upweke ambao angebakia nao Tracy, kwani walishazowea kuwa wawili toka tumboni, nimelia hadi hapa ofisini wamenishangaa, nimejihisi ni mimi kabisa, Violet, MSHUKURU MUNGU MDOGO WANGU, pia nimejifunza kitu toka kwako,
    NIMEJIFUNZA IMANI,
    pole na hongera kwa kukuza mama, siku moja nikija dar ntakutafuta nimpatie Tymon zawadi,
    nimeguswa sana. kwasasa niko UK
    TASREEEN

    ReplyDelete
  6. Pole sana dada na hongera kwa kuwa na imani endelea kuamini kwa Mungu anatenda.

    ReplyDelete
  7. Pole sana Amanda kwa kumpoteza Baba, Mungu akupe nguvu,
    WAPENDWA, HUWA napenda kuomba maombi ya kuweka NADHIRI, hivyo baada ya kutoka hospitali tu! nilitoa sadaka ya shukrani Kwa Mungu wangu
    ASANTENI

    ReplyDelete
  8. Mungu akubariki sana mama T endelea kuwa ushuhuda katika maisha yako mshike sana yesu ng'ang'ania sana imani endelea kuwafunika watoto wako kwa damu ya yesu ili adui asipate nafasi, Binafsi sitasahau kaka yangu mpenzi na rafiki yangu alipokufa katika Ajali ya basi la No Challenge maaneo ya msangazi muheza walikufa basi zima lakini ukiangalia maeneo waliofia kama ilikuwa nguvu za giza akaacha mke mjazito baaba ya siku ishirini mtoto akazaliwa, huwa nikikumbuka kifo chake huwa naumia sana nikikumbuka mazishi yake tulimzika akitoka damu puani masikioni mdomoni huwa inauma lakini namshukuru mungu katuachia binti aitwae Witness yuko darasa la sita sasa lakini mungu ni mwema kila anachokifanya kwetu ni chema kabisa, Ila ninachojua mungu hakutuimbia misiba wala huzuni, mungu ni mungu wa furaha amani, na ushindi.basi dada v nakupa kamstari zab 105:1-5
    Mpendwa

    ReplyDelete
  9. POLE VIOLET
    MIMI SITASAHAU SIKU NILIYOMKUTA MUME WANGU WA NDOA AMELALA NA HOUSEGILR WANGU KITANDANI KWANGU
    sijui kwanini nashindwa kusahau japo nilisamehe, nilimkuta mume wangu live na housemaid wetu, tena nilikua natoka safari, nilifiwa na mjomba wangu, nilipata lift na kurudi nilitaka kumfanyia suprise, nilichokikuta
    mh! najuta mwenzio, sijui kama nitakuja kusahau, sijui

    ReplyDelete
  10. KAMA NI MIMI HUYO NESI WALA SIMSAMEHI,
    LAZIMA NINGEMKOMESHA!
    WE! ANIULIE MWANANGU HIVIHIVI, UNA MOYO DADA

    ReplyDelete
  11. Kusamehe mpenzi wangu ni lazima lazima usamehe ili mungu aweze kukupigania na kuingilia kati mambo yako usipomsamehe nesi wewe ni mangapi umefanyia wenzako au kwa mungu mbona mungu amesamehe, kama huna mungu hutasamehe, lakini kama una mungu utasamehe kwa mungu kuna msamaha ili mungu agopwe bwana angehehesabu maovu nani angesimama
    mpendwa

    ReplyDelete
  12. Pole sana mama Tracy,yn wakati nasoma nlihic km ndo naona picha yenyewe,inackitisha sana,pole mumy.ASIA ALAWI

    ReplyDelete
  13. Pole sana inatia simanzi!

    ReplyDelete
  14. Pole sana yaani sina hata lakusema, mshukuru Mungu,

    ReplyDelete
  15. pole sana rafiki,inabidi utumie busara sana kumlea na kumpenda zaidi,na uache tabia ya kumpipiga zaidi usiwe mkali saaaana kwa watoto boazy hapa

    ReplyDelete
  16. hahaaaaaaaaaaaa
    wewe boazy wewe,
    mh! ndio unanipaka??? kichapo lazima kitembee tu! na wananijuwa, sitaki ujinga, wakikosea mara ya kwanza nawaambia, mara yapili kichapo,
    ahhahahaaaaaaaaaaaaaaa, mtoto asionywa kwa kiboko, hata tabia zake zinakuwa haziko katika mstari, mii mwenyewe nilichapwa sana tu!

    ReplyDelete