Friday, February 26, 2010

SIWEZI KUTULIA NA MWANAUME MMOJA - NISAIDIENI

Jamani, nina shida kubwa sana, ambayo hata sijui kama nitakuja kuepukana nayo, na kwakuwa mficha uchi hazai, nimeona niseme ili nisaidiwe, mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 27, nimezaliwa na kukulia UK, ambapo ndipo alipokuwepo mama yangu, baba alishafariki wala sikuwahi kumuona

nilipomaliza elimu ya secondary nilikuja tanzania kwa aunti zangu ambao tunaishi nao hapa Mwanza, Nilikaa kwa aunt zangu, wakati nikiwa kwenye process za kutaka kurudi kwa mama, bahati mbaya mama yangu alifariki, hivyo sikuweza kurudi tena kule, na kuamua kubaki tanzania kwa ndugu wa mama yangu

hapo nilikuwa ninamiaka  23, nilifanikiwa kupata kazi airport, nilifanya kwa muda wa mwaka mmoja tu, nikapata mchumba, ambae alinipenda sana, na aliahidi kunioa, basi nami nilimpenda sana, nilimtambulisha kwetu akajulikana, na kwao alinitambulisha, kabla ya kufunga ndoa nilipata ujauzito, ambapo familia yangu iliamua nizae ndipo nifunge ndoa, ikawa bahati mbaya, kabla yakujifungua nilipata kifafa cha mimba, hali ambayo ilisababisha mwanangu afariki,

nililia sana, tokea pale mchumba wangu akasafiri kwenda kusoma, na kudai nisubiri arudi ili tufunge ndoa, ajiandae vizuri, nilikubali, lakini aliposafiri tu! mawasiliano yalikufa, wakwe zangu wakaanza kunidharau, nikienda kwao nikama mzigo, hali hii ilinisumbua sana, kwakuwa nilimpenda sana mchumba wangu, nimekaa mwaka mmoja, nikapata taarifa kwa watu kuwa mchumba wangu anao, na vikao teyari,

niliumia sana, nakumbuka nilikunywa sumu kabia, mama mdogo aliniwahisha hospitali, nikapona, sasa tokea hapo, mimi sikuwa nikitaka mwanaume wa kunioa, wachumba walikuja niliwakataaa, nikawa kama niliechanganyikiwa vile, sasa hali ile hadi leo nikikumbuka, nalia sana,
TATIZO NI HILI,
niliamua kuwa na boyfriend, ambae nae tulidumu nae kidogo tu, akaniacha, baada ya muda mfupi nae akatangaza ndoa na mwanamke mwingine, hapo ndipo nilichoka kabisa,
niliwadharau wanaume wote, waliokuwa wakipita mbele yangu, nikawa nalala nao hovyo tu, hakuna niliempenda, akinitaka nikimtamani tu! nalala nae,  siku moja , ya pili nakuwa sihitaji kumuona kabisa, na simu yake naweza hata kudelete,
hadi sasa sijui nimefanya mapenzi na wanaume wangapi, NA SIWEZI KURUDIA KULALA MARA MBILI NA MWANAUME MMOJA, siwezi kabisa dada, yani kabla ya tendo lenyewe, nakuwa na hamu nae sana, nikimaliza tu! namchukia kupita kiasi,
dada, niko kama kahaba fulani hivi asijuwa muelekeo wake, yani napenda sana kufanya mapenzi na wanaume tofauti tofauti, sio mmoja, familia hadi imeamua kunitenga, maana ninayofanya ni uchafu sana, nimepoteza muelekeo wa maisha yangu, nikaamua kuja dar es salaam, nikapata kazi hapa ........... napo hadi sasa toka nije sijui nimetembea na wanaume wangapi, kila atakaenijaribu tu! nammaliza, niko teyari kufata mapenzi hata mikoani, nikishafanywa tu! narudi natulia,

kipindi cha mwanzo nilikuwa naona sawa tu, nilijitambua kama mimi ni malaya, sikuwa tayari kupima hata ukimwi maana nilijuwa ninao, lakini cha kushangaza, kuna siku niliumwa sana nikiwa geto kwangu, rafiki yangu alinishauri twende hsptl nilikataa kabisa, baada ya kuzidiwa sana, nikasema liwalo na liwe, nikapelekwa hospitali, katika vipimo walivyopima, damu yangu ikawa iko safi, sikuamini kabisa, hapo hapo niliona nimepona, nikawa na malaria tu!

baada ya miezi mitatu nilirudi kupima tena, nikakutwa safi, hadi sasa idadi ile ya wanaume imeshuka sana,
lakini mbona naona nateseka sana? nakuwa na hamu sana ya kufanya mapenzi, hadi naota kabisa nafanya mapenzi, hali hiii inanipa shida, sijui kama inatibika, natamani kuwa mtu mwenye heshima, natamani kurudisha heshima niliyoipoteza, natamani kurudi na kuanguka kwa ndugu zangu ili wanipokee upya, ila sijui kam nitaweza nimeshazowea, nisaidieni walimwengu.





5 comments:

  1. Pole mdogo wangu kwanza mshukuru mungu kwa kukutendea muujuza, wewe una pepo la uzinzi kabisa sio wewe tafuta makanisa uwende ukaombewe mapepo yakutoke na mungu aondoe kiu ya kufanya ngono unajua hakuna kiu ambayo mungu hawezi ondoa,ikibidi ufanyiwe maombi ya Derivarence, kama uko Dar nenda Buguruni kwa mzee Salu huduma ya nyumba kwa nyumba Buguruni malapa nyuma ya hosteli na upone majeraha ulioumizwa na wanaume, na uweze kurudisha thamani yako.

    ReplyDelete
  2. dada violet, huyo dada namjua, amakweli watu wanaweza kubadilika, namjua hadi jina lake, na aliwahi kutembea hadi na shemeji yangu,
    kama kweli umeamua kutulia ni jambo la kheri, lakini sijui kama utaweza, maana mh! wewe ni kiboko,
    dada violet, huyo ni mschana ambae kama akitulia anapata mume mzuri kabisa, maana yeye mwenyewe ni mzuri sana, ana asili ya uafricast fulani hivi, ni mzuri sana, watu huwa tunashangaa anahangaikia nini, hata ukikaa nae tu story zake ni mapenzi,
    kwakweli msaidieni jamani, labda atabadilika kwa kuwa kaamua mwenyewe

    ReplyDelete
  3. pole sana dada,nakushauri ufanye uamuzi wa kumrudia mungu akuondolee uchungu ulio achiwa na mchumba wa mwanzo kabisa,pili ujisamehe ww mwenyewe na kuweza kufanya hivyo inabidi ukubali kwamba bwana yesu alimaliza yote pale msalabani na hakuna lisilo wezekana kwake wala,unajiona kama vile huna thamani lakini unathamani sana mbele za mungu na kama ukimkimbilia atakubadilisha kabisa na kuwa kiumbe kipya,tafadhali anza kwenda kanisani na maisha yako yatabadilika jumla kabisa,Mungu akubariki sana kwa maana ni mwema kwetu sote na hakuna dhambi kubwa wala ndogo kwake anatupenda sote dada yangu wala usikate tamaa .love u sister.julie

    ReplyDelete
  4. pole sana na matatizo lakini kama uko serious naomba nitafute mimi natafuta mchumba wa kuoa na nashkuru nini kila kitu mungu amenipa uwezo wa ktosha ila natafuta mke ambae anejua matatizo na imani wewe utatulia kama utakua na good time kama uko tayari nitumie email yako kwenye comments humu alafu mimi nitakutumia yakwangu bye

    ReplyDelete
  5. nitafute mimi nitakutomba na kukufira mpaka utaweza kutulia kwangu!

    ReplyDelete