Saturday, May 29, 2010

KINA BABA MSIOKAA NA FAMILIA ZENU- HEBU JARIBUNI WEEK END HII TUONE MTAPUNGUKIWA NINI

(wapenzi wangu, nitajitahidi kila weekend tuwe tunaongelea mambo ya kifamilia hasa kwa upande wa malezi kwa watoto wetu, pia nitoe nafasi hii kwa yeyote yule mwenye kitu chochote cha kumfanya mtoto ajisikie vizuri, basi anitumie kwenye email yangu pale juu, ili aweze kushare nasi, tunajisahau sana juu ya suala zima la watoto wetu.)









Jamani kuna kitu kinasumbuwa familia nyingi sana, nakutana na watu wengi hasa wanawake nikiwa salon na sehemu zingine, wanalalamika sana kuhusu waume zao kutokutulia nyumbani siku za weekend, unakuta mtu yuko busy kuanzia jumatatu hadi jumapili, kazi na yeye, yeye nakazi, sasa sijui ndio kazi kweli au ndio kazzzzzziiiiiiiiiiiii


inapendeza kuona familia zikiwa na furaha kwa pamoja, sio kila siku, but hata weekend moja moja jamani
chukuwa mkeo, watoto wenu, nendeni sehemu ambazo mtabadirisha mazingira ya nyumbani kidogo, japo kwa masaa machache, hebu jaribuni weekend hii muone watoto watakavyofurahia,

si lazima beach tu jamani, nendeni hata sehemu yenye hewa nzuri, ukiwa na familia yako, na mkeo inanoga jamani, mtakaa mtacheza na watoto kidogo, mtawauliza maswali ya michezo michezo, yani inapendeza sana,
lakini unakuta mwanaume mwingine, unapita hata mwezi hajuwi kama mtoto shule anaenda, anaandika, anashida gani, hajui lolote, akitoka kumi na mbili akirudi saa tatu saanne, wakati mtoto amesha lala, sijui wanafikir sifa

watoto ni wepesi sana kuridhika, chukuwa kipesa chako kidogo, wapeleke hata super market tu! wakajichagulie wanachotaka, mkimaliza mnakaa mahali mnapata chakula au hata kinywaji, then warudishe nyumbani, kweli siku hiyo mtoto ataenjoy sana, sio mtoto ametoka sana, kaendashule, akirudi kucheza cheza nyumbani, wala hainogi, na hii huzidisha sana mapenzi kwa watoto wetu, sio unakuwa busy kiasi kwamba siku ukishinda nyumbani tu! watoto wanakushangaa na kumuuliza mama, ''baba anaumwa''
hebu jaribuni jamani, muone watoto watakavyojiskia vizuri,




1 comment:

  1. wape wayapokee hao, wamezidi lo!
    mume wangu mimi hadi watoto huwa wanauliza mama hivi baba amesafiri, yani dear, ni kama ulikuwepo vile

    ReplyDelete