Wednesday, May 19, 2010

KILA NIKIFANYA NAE MAPENZI- NAPATA MAUMIVU MAKALI SANA


Dada violet, pole na kazi, nahitji msaada wako kama utaweza kunisaidia nitakushukuru sana, pia kama inawezekana weka kwenye blog yako (ila usinitaje jina) ili niweze kupata ushauri zaidi,

Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 22, niko Zanzibar, tangu niwe mwali hadi leo nimekutana na wanaume wawili, mmoja aliniacha, kwa sababu ambazo hata sizielewi Mpaka leo hii na alinitamkia kabisa sina sababu ila tu sikutaki tena, iliniuma sana nilitamani hata kujiua, ukizingatia niliweka nadhiri kuwa atakaenibikiri ndie atakaenioa, lakini akawa ameshapotosha ndoto zangu,

Baada ya muda nikiwa chuo, nilipata boyfriend mwingine, ambae niko nae hadi sasa, cha ajabu kila ninapokutana nae, tukimaliza tu! Huwa naumwa sana hadi nameza dawa, yani akishaniambia kesho tutafanya mimi nitalala nawaza usiku kucha, Napata maumivu makali sana huku chini na maeneo ya kwenye kinena panauma sana, huwa naumia hata saa zima na jasho linanitoka kabisa

Huyu boyfriend wangu hadi anaogopa kunigusa, sasa nawasiwasi asije akashawishika kuwa na mwanamke mwingine, nampenda sana, na hata kwetu wameshamjua bado kuja rasmi tu!,

Aliwahi kunichukuwa kunipeleka hospitali moja huku huku Zanzibar, dada violet nilipimwa kila kitu, lakini hakukuwa na tatizo, hata daktari alishangaa, yani alichukuwa vipimo vyote, lakini hakukuwa na tatizo, siku ingine tena tulisafiri nae kwenda Kigoma, tulipofika tulilala pamoja hotelini, alivyonifanya tu! Sikulala hadi kunakucha, kiuno kinauma hadi miguu, asubuhi alinipeleka hospitali kule kule kigoma, napo wakaniambia kuwa sina shida

Tukakaa kama wiki mbili baada ya kutoka hsptl tukafanya tena, maumivu pale pale, nikaenda hospitali ingine tena kwa mara ya tatu, napo wakasema kuwa mimi sina tatizo lolote, wakampima hata na boyfriend wangu wakasema pia hana tatizo,

Hadi sasa sijielewi, maana nakosa kitendo cha muhumu kuliko vyote, naumia sana na hasa wasi wasi wangu ni kwamba huyu boyfriend wangu atanikimbia, Napata taabu sana naombeni mnisaidie nifanye nini? nawaza labda tatizo linaweza kuwa kwangu ndio maana hata mwanaume wa kwanza alinikimbia bila sababu



6 comments:

  1. pole mdogo wangu,
    nachoona hapa mimi kwa upande wangu ni kwamba yawezekana huyo ulienae ndie mwenye shida,
    nasema hivyo kwakuwa nilikuwa na rafiki yangu alikuwa na mchumba wake, ane walikuwa wakifanya tu! anumia sana hadi analia, lakini walipokwenda hospitali ikaonekana yule mwanaume akaonekana ana MASHINE ndefu zaidi, alichoniambia rafiki yangu ni kwamba yule kaka alivalishwa pete, KITU kikawa saizi yake, na mchezo ukaendelea kama kawaida, (kwani kwa yule wa mwanzo ulikuwa ukiumia pi)
    kingine yawezekana maandalizi yenu si mazuri,
    mapenzi yanatakiwa kuandaana, muandae kwa muda mrefu nae akuandae kwa muda mrefu, mawazo yako yoteeee, yaweke pale, jiachie, hata kama ulikuwa na hasira, basi hapo weka pembeni kwanza, akili yote iwe hapo, nae pia afanye hivyo, inaweza kusaidia kulainisha maungo yako na mambo yakaenda kama kawa, nisichimbe ndani sanaaaaa, ngoja niwaachie na wengine tusikie maoni yako kwako.

    ReplyDelete
  2. hamjui kuandaana kama alivyosema violet
    we mrambe, mfinyangane hata saa zima, au inawezekana mmoja wenu anamwonea kinyaa mwenzie, ndio maana ushirikiano unapungua
    pole mwaya, kuukosa uroda, ni mateso

    ReplyDelete
  3. pole mdogo wangu, nakushauri uombewe yawezakuwa ukawa hata na pepo la mahaba linalokuchosha usiku wakati wewe hujui, tena huko pwani ndio yamejaa sana, usiku yanamaliza hamu zao, asubuh unakuwa huna hamu na unapoteza hamu ya mapenzi pole we!

    ReplyDelete
  4. Pole sasa sana mdogo wangu, inawezekana huyo boyfriend akawa ana uume mkubwa zaidi kuliko maumbile yako, lakini hujatuambia huyo wa kwanza kama mlikuwa mkifanya mapenzi unaumia, ebu tufafanulie hapo kwanza, pia mapenzi yanahitaji utulivu, namaanisha maandalizi kila mmoja anatakiwa amuandae mwenzake kikamilifu ndio mfanye lakini siyo kukurupuka tu ili mradi, mimi nina swali, je huyo bwana unampenda kutoka moyoni? maana mtu unayempenda hata akikugusa tu wewe uko chini hoi, kwa upande wangu mimi ni hivyo sijui wengine, pole sana kwa kukosa raha ya muhimu kuliko vyote duniani

    ReplyDelete
  5. Ushauri wangu ni kuwa,
    Fanyeni uchunguzi wenu kujua ni sehemu gani hasa chanzo cha matatizo kama ipo.

    Mwambie akija siku nyingine, mfanye romance tu mwanzo mwisho uangalie mwili utakuwa katika hali gani.

    Hatua inayofuata anaweza kucheza na kufanya kijuu juu tu, labda aingize kichwa hivi. Ikitokea hamna maumivu, hiyo inaweza kukuondolea hofu ya kitendo, huenda utajikuta unahitaji achezee zaidi hata atakapokuja kuingiza hutagundua na utakuwa mwisho wa hofu yako.

    yangu hayo kwa sasa!

    ReplyDelete