Monday, March 1, 2010

MUME WANGU ANATAKA STYLE ZA MAPENZI ZA AJABU-ZINANIUMIZA


Hujambo violet, mimi ni mama wa miaka 36, nina watoto watatu, nina miaka tisa kwenye ndoa, tulipoona na mume wangu tulikuwa tukifanya mapenzi style za kawaida tu, tunabadili style lakini ni zile za kawaida

Umefika miezi mwala sasa mume wangu amebadilika sana, yani hatulii yani mimi nayeye hatukai nusu saa bila ugomvi, kitu kidogo tu, hasira kwangu na anapeleka hadi kwa watoto wangu, yani hadi wanamuogopa sasa hivi, wakimuona tu! Wote wanaenda kulala,


Hadi sasa nahisi mume wangu anamwanamke nje, tena ni Malaya kabisa, maana violet mdogo wangu, mume huyu huwa nakaa namfikiria naona kama wamenirogea vile, hajui kubembeleza kwenye mapenzi, yeye ni kuamrisha tu, tofauti na zamani, hata mimi nikimbembeleza labda nimshike shike sehemu ambazo najua akishikwa anafurahi, nimnyonyenyonye hapa na pale, zamani alikuwa anapenda sana. Siku hizi hataki kabisa, nikianza tu, anasema ah! Nimechoka mimi, kwanza nimeshaoga unanipaka matemate yako, wakati bafu liko hapo chumbani angeweza kuoga tena,

Sasa kuna kipindi nami niliamua kukaa kimya, nikawa nasubiri hadi yeye aanze, lakini sasa style alizokujanazo sasahivi mimi siziwezi, yani sio za kawaida, nina mwili mkubwa, nilizaa kwa operation, nina kovu tumboni, siwezi kujikunja kunja Napata maumivu, sasa yeye utakuta ananikunja kama samaki, yani nabanwa nakuwa mdogo, nalia sana, sio kwa raha ila ni kwamaumivu, na hata nikilia anasema nisubiri hadi amalize ndio aniache, akiniacha tu! Ujuwe lazima nitalala hata siku mbili, naumwa sana kiuno,

Kuna siku nilimuuliza kwanini ananifanya kama ananibaka vile, akasema akifanya style za zamani hasikii raha kabisa, kuna kipindi alianza kuniambia kuwa anataka anifanya nyuma, sikuamini masikio yangu, nililia sana, nikamwambia ndoa na ife, narudi kwetu, akanisihi nibaki, nashukuru hakurudia tena kutamaka ushenzi huo,

Style zake za sasa hivi sijui anazitoa wapi, yani sasahivi akiniambia kama anahitaji tu! Basi naweza meza hata dawa ili nijifanye naumwa, napoteza furaha kabisa, yani hawezi kabisa kunifanya kawaida, naombeni mnishauri nifanyaje, maana ni kweli kwa mwanamke yeyote Yule style ninazofanywa mimi, lazima angelia, mimi hadi huwa nakwenda hospitali, ila nikifika sisemi kama nimefanya style mbaya, huwa nadanganya maana naona ni aibu, nitamuaibisha mume wangu na mimi pia.





 

10 comments:

  1. Ney or Mumy BrendaMarch 1, 2010 at 10:39 PM

    Dah!!! pole sana mama yangu hayo ni mapito tu ya dunia jipe moyo utashinda mama kumbuka kila jaribu lina mlango wa kutokea wewe piga goti Muombe Mungu ukiamini kwamba hakuna neno gumu lolote asiloliweza, Huyo ni pepo amemuingia mume wako na kama ulivyosema ana mwanamke mwingine so ameshafanya mapenzi nje ya ndoa tayari ameshaweka agano mama yangu hapo lazima uvunje nguvu za giza. Omba mama mshike huyo mwanamke kwa imani mkatilie mbali mwagie damu ya Yesu akimuona mume wako akose amani na mume wako mshike kwa imani omba mwagie damu ya Yesu yani akitaka tu kwenda kwa huyo mwanamke asikie kukosa amani na hivyo viungo vyake vileegee ktk Jina la Yesu hayo yote mama yangu yanawezakana ukisimama ktk maombi utaonyeshwa nini kinaendelea hadi uatashangaa mumeo anaweza kukuona kama wewe ni mchawi ila uchawi wako uko kwa Yesu.Omba mama usichoke utashinda!!!
    Wako Mumie Brenda

    ReplyDelete
  2. Mpendwa Pole,kwa maelezo yako inaonekana unaumia sana.
    Ningependa kukushauri kama ifuatavyo:
    -umesema haipiti nusu saa ugomvi hadi watoto wanamchukia baba yao,jaribu kubadili kauli wakati wa maongezi,miaka tisa mlioishi pamoja mtakuwa mnajuana sana,na hii ni kitu kizuri jaribu kumfanya mume wako awe rafiki yako..kuwa mcheshi,mtundu na sometimes mtani..plan au ratiba ya nyumbani ibadilishe..ikiwa ni ileile kila siku inachosha..kama unapenda kwenda beach panga nae akikataa nenda na watoto,..akiona unatoka atapata WIVU mapenzi bila wivu kiasi yanapotea
    -wakati watendo anakukunja kama samaki na anasema subiri ni malize;hapa hamna love jamani,tendo lile nikila mtu anatakiwa afurahi kama wewe unalia yeye anasema subiri...kwakweli kama ni mimi ningempiga kofi...sasa sijaelewea maumivu yako ni kwamba hajakuandaa hivyo anaingia tu kabla ujawa tayari au ni hiyo mikunjo anayokukunja?kama ni maandalizi..jaribu kuwa creative..sio lazima yeye akukunje tu,kuna style ya side by side,unaweka cross miguu yako unakuwa kama umebend kwenye kiuno kidogo then unabana kidogo na kuachia(zoezi la haja ndogo kama walijua)unaachia na kubana,mbona ataenjoy tu tena ataanza kulia yeye sasa..vilevile vifutio vyetu vikoje?kama unatumia tissue acha mara moja...nunua taulo ndogo tena jeupe...uwe na kibeseni kidogo na thermos special yenye maji vuguvugu mfute vizuri..nawe jifute na maji vuguvugu...yani akikugusa tu na hilo joto la vuguvugu atataka tena ghafla….kama anapenda movies jaribu kutafuta movie nzuri za mapenzi..siyo hard core...angalieni kwa pamoja atabadilika tu..mume wako anakupenda na anapenda kufanya mapenzi na wewe ila tu approach anayotumia siyo sawa...so use the opportunity kuwa creative,mapenzi ni furaha...tafuta hata cd ya mziki nzuri weka,badilisha chumba chako,weka fresh flowers...badili position ya kitanda ili mradi tu mandhari ibadilike...kukiwa hivyo hivyo..style hiyohiyo lazima atachoka nawe utaendelea kuumia kulia kwenda hospital..hospital twende kwa maradhi na siyo kwa maumivu ya style za mapenzi.
    Yote haya yafanye ukiwa umemweka MUNGU mbele,kila jambo lenye nia njema na bwana atalibariki...ubarikiwe sana,

    Nitty..

    ReplyDelete
  3. dada v, ugomvi wangu mimi na wewe uko pale pale, ni kwanini na wewe hutoi maoni yako? tukaona busara zako? wewe unatupostia tu! then unakaa kimya, mimi nafikiri ingekuwa nzuri sana kama wewe ungekuwa wakwanza kupost kuliko kukaa kimya, sio nzuri hii
    take action haraka iwezekanavyo

    wewe mama, mumeo amekuchoka, hakuna lolote, hakuna cha maombi wala nini, huyo hata umrambe hadi m.... atakufanya kwa kukubaka hana lolote, kesha zowea kufanya na machangu huko, sasa zile style ndio analeta kwako, mwambie akome, nakushaur ongea nae wewe kwanza, kama aliweza kukusikiliza kuhusu kukufanya nyumba, basi hata hii raugh sex yake anaweza badilika, akiwa jiwe, muitie watu,
    babu mapenzi kufurahia, ni hisia, kila mtu amridhishe mwenzie, lo!
    TAMIA

    ReplyDelete
  4. ukituupdate kama hivi, wala hata Hatutakusumbua dada, wengine hatujaolewa, lakini tunajifunza sana
    mama ulietoa mada, pole kwa shida hiyo, huyo mumeo atakuwa ana mapepo ya umalaya, hivi umeona cd za wanawake malaya wanavyofanywa? wanakunjwa, sana ila wao wamezowea, na wanafanywa vibaya kwakuwa wale si waume zao, wanapita tu,
    wanaume wafikirie na hili, kuna raha gani wewe kumaliza kabla ya mke wako, na bado anakulala mikia kuwa anaumia, sijaolewa ila nishawahi kuishi na mume miaka miwili, tukashindwana tabia kila mtu akaambaa kipango wake, kwanini umuumize mke wako? kwanini umfanye isivyotakiwa wakat unajua anamatatizo, mwenzio ana operation wewe unamkunja,
    ni dhambi, TENDO LA NDOA NI TENDO TAKATIFU AMBALO LIMEKUBALIWA NA MUNGU, sasa utakatifu unatoka wapi wakati mwenzio anaumia hadi kwenda hospitali, ni tabia mbay, pia ni kumnyima haki yake mke wako, jirekebishe,
    huu ni unyanyasaji kabisa, mkeo wa ndoa utamuombaje TIGO? mke ukiombwa tigo ujuwe hupendwi, na unadhalilishwa, ikiwezekana umshtaki, wanaomba wake zao TIGO WOTE WAPUMBAVU.
    MKOME KUTUDHALILISHA, Violet, nahitaji kukuona, niko dar es salaam, ofisi zangu ziko kijito nyamya, nataka kuongea na wewe, ni muhimu ni serious kwa faida yako, yangu, ya jamii hasa upande wa wanawake,
    namba yangu nakutumia kwenye simu yako sasa hivi

    ReplyDelete
  5. Si afadhali ya wewe unaekunjwa mi nalala na mume wangu kitanda kimoja na hajanishika hata ziwa huu mwezi wa 3.Fanya mazoezi sio upungue bali kulainisha viungo ukunjike bila kuumia(stretching).Hilo la jamaa kutaka kumaliza tu kuwa mbunifu kwa kechezea kisimi chako akiendelea na shughuli ili nawe ufike na kuinjoi mchezo.

    ReplyDelete
  6. mh hiyo ni balaa maa mbaya zaidi anaweza kukusababishia matatizo makubwa mimi tu sijazaa na nikifanyiwa hivyo nalia, pole mama

    ReplyDelete
  7. pole sana ila nadhani nawewe lazima uwe mbunifu kwani mapenz nayo hutaka ladha tofauti kidogo, pia naungana na mseji moja kwamba nawe jitahidi kufanisha mwili mazoezi ili upungue japo kidogo, pia jitahidi kuwa kimapenzi pindi jamaa anapotaka.

    ReplyDelete
  8. huyo mwanaume n fedhul xana lkn jipe moyo mama yangu kwan hakuna marefu yasiyo kuwa na ncha jarbu kukaa chin na mumeo umwambie n namna gan unavyojickia akishndwa kubadilika fikisha suala hl kwa wazaz

    ReplyDelete
  9. dah, wanaume wengine bana, mtu kajifungua ana oparation nas kidonda hakijapona vizuri anaanza kumkunja na kutaka mastail yake aloiga kwa changu wake.....kuweni na huruma jaman, kila mtu anapenda mapenz na anapenda afurahie, sasa nn kutesana, ndo maana wengine wanaamua kujitafutia na wao vijana wao wakuwapa mapenzi wakibembelezwa, mwanamke mbembeleze kitandani uone jinsi atakupa dose.....khaaaaaa

    ReplyDelete
  10. Μagnificent beat ! І would liκe to apprеnticе whіle yοu amend youг wеb sitе, hoω сan i subscribe
    for a blоg site? The аccount helpеd
    mе a acceptable deal. I had been tiny bit аcquainteԁ of this your bгoadсast provіdeԁ brіght сlеar concept

    Here is my blog - http://5htp.tv/griffonia-simplicifolia/
    my web site :: http://5htp.tv/griffonia-simplicifolia/

    ReplyDelete