Sunday, March 14, 2010

HAPPY BIRTHDAY MY TWINS (TYMON & TRACE)

This saturday ilikuwa ni birthday ya watoto wangu, wamefikisha miaka minne, hahahaaaaaaaaaa, nimekuza jamani lo! nikiwatazama narudisha sifa kwa mwenyezi Mungu, nikiangalia mapito niliyoyapita toka nilivyowazaa, hadi sasa wamekuwa hivi, huwa sometimes siamini kabisa. (4 years now) Namuomba Mungu awape afya njema, awakuze wanangu
Huyu ndie Binti yangu (kurwa - TRACE)

Na huyu ndie Kijana wangu  (Doto - TYMON)

Dadaa kaweka pozi, we!

kama kawaida, haiwi birthday bila kuwepo keki, hii ni ya Trace

Nahii ni ya Tymon, was simple but fun!

walizma mishumaa, kwa pamoja

Na kila mtu alikata keke yake kumlisha mwenzie, hahaaaaaa raha jamani da!

Mh! kazi ipo hapa, huyu trace hizi pozi sijui anazitoa wapi, du!

hawakuwa wachoyo, waliwaalika na wenzao, atleast wawaimbie
(asieimba hali keki, aseimba haliiiiiiiiii)

At the end, nilipata picha moja na wanangu ya ukumbusho, mh! pozi za picha ndio sina kabisa yani, lo!
all in all, tulimaliza salama kabisa, Naomba mwenyezi Mungu awape maisha marefu kabisa, awalinde, awatangulie kwa kila kitu, wakafanyike baraka kwa kila mtu, akawaepushie yote yaliyo mabaya, na kuweka rehema nyingi juu yao, (ASANTE MWENYEZI MUNGU KWA ZAWADI HII)
STAY BLESSED MY LOVELY TWINS


.

10 comments:

  1. Amen! Violet, Mungu atakukuzia tu! kwani hamtupi mja wake, nimetamani kama wawe watoto wangu, nahisi ndio ningefunga na uzazi, staki hata kuzaa tena, wazuri, trace amenifurahisha pozi zake za kimodel model,
    NAOMI

    ReplyDelete
  2. Hongera dada violet!watoto wako wazuri na wanapendeza sana.Mungu awatunze na kuwakuza.Dada violet kitu kimoja ambacho hujatenda haki ni baba watoto hujamwonyesha.Angalau basi picha ya pamoja na watoto wenu shostiiiiii unaniangusha.

    ReplyDelete
  3. kweli mwenzangu, dada violet hapo umechemsha kutomuonyesha baba watoto. au hakuwepo? hahahaaaaaaaaaa!! Hongera sana kweli umekuza. KUZAA KUZURIIIII!! Mungu akutunzie.

    ReplyDelete
  4. hahahaaaaaaaaaaa, lo! ndio mnanipasha??
    baba yao alikuwepo, ndio alikuwa mpiga picha wetu, but nilipomwambia nimpige na yeye na wanae, akakataa, lakini kwa ujumbe huu nayeye atakuwa ameusoma, next birthday tukiwa hai, atapiga na watoto mtamuona together with his kids, msikonde maswahiba wangu, (ila nanyie ni wambea kha!)

    ReplyDelete
  5. Hongera sana, mungu akutunzie. Kwakweli unabahati sana kupata mapacha na jinsia tofauti,rahaaaaaaaa.Mimi nimeolewa ila bado sijabahatika kupata mtoto ila huwa na muomba mungu sana anipe mapacha kama hao wako wakike na wakiume,huwa natamani sana hiki kitu kwenye maisha yangu.Violet, uniombee na mimi nipate mapacha kama wako,ni faraja isiyokifani.Ubarikiwe sana

    ReplyDelete
  6. Mpendwa wangu hapo juu, asante mpenzi, na nikweli kabisa kuwa na watoto twins tena jinsia tofauti, ni raha sana,japo wakati wadogo nilipata nao shida sana, maana walikataa kunyonya mapema sana, basi we! full tafrani yani, But thanks God, anawalinda kila iitwapo leo.
    MPENDWA WANGU, ALWAYS HUWA NAPENDA SANA KUMWAMINI MUNGU! NA NAAMINI KUWA KUAMINI KWAKO NDIO MUUJIZA WAKO,
    wewe muombe Mungu tu, atakupa mpenzi, ila tu! kama hutamtilia Mungu mashaka, uamini kile unachoomba,
    NA IWE HIVYO,
    AMINA MAMIE

    ReplyDelete
  7. Hi violet wanao wazuri dah wa kike ana pozzz si mchezo, nawapenda wazuri kama mama yao

    ReplyDelete
  8. best wadau saa ingine wambeaaaaaa duh! napenda ulivyowajibu hahahahahahahaaaaaaa

    ReplyDelete
  9. HONGERA SANA MAMA WAWILI KWA WANAO KUTIMIZA MIAKA MINNE. MUNGU AWALINDE NA AWAJAALIE AFYA NJEMA. MI ANITHA WA DOM. MPE HI MAMA GOD. NIMEWAONA TYMON NA TRACE WALIPENDEZA HALAFU WANAONEKANA WAKUBWA. HONGERAAAAAA.

    ReplyDelete
  10. thank you very much Anitha, thanks for the sweet words to my kids, wameshakuwa sasa, inabidi nianze kuwaza wadogo zao wengine shost hahaaaaaaaaaaaa,
    ill send ur greetings to Mama God, stay blessed!

    ReplyDelete