Thursday, June 24, 2010

NILIWAHI KUINGILIWA KINYUME NA MAUMBILE, NIKIZAA MUME WANGU ATAJUA?

habari aunt violet hongera sana kwa kuanzisaha blog ambayo inasaidia watu wengi kwa ushauri mungu akuzidishie.mimi ni msichana mweye umri wa miaka 25 nimeolewa mwaka jana naweza kusema tangu nimeolewa karibu mwaka sasa na nashukuru tunaishi vizuri na mume wangu.

Tatizo langu ni moja aunt kabla sijaolewa niliwahi kuwa na boyfriend ambaye nilikuwa nae kwenye mahusiano karibu mwaka mmoja mwanzo alikuwa anaonyesha ni kijana mtaratibu na mstaarabu lakini baadae kama baada ya miezi sita ya mahusianao alianza tabia ya kuniomba tufanye mapenzi kinyume na maumbile, Sio siri nilipingana nalo sana hilo jambo baadae akaniambia alikuwa ananitania aone kama nitakubali yakaisha.

lakini baada ya kama miezi kadhaa hivi akaanza tena kuniambia kuhusu jambo hilo tena nikakataa, siku moja tukiwa tunasex akaforce kuniingilia kinyume na kwakuwa alinistukiza akaniingilia tukawa tunagombana huku mimi nikijitoa nikafanikiwa kutoka huku nikiwa na maumivu sana kiasi kwamba kama muda wa siku tatu hivi niliumwa nikastop mawasiliano nae

akaanza kunifuata kwetu na kunipigia simu akiomba turudiane nimsamehe ni shetani alimpitia alinibembeleza sana kwakuwa nilimpenda nikakubali tukaendelea na mahusiano siku nyingine tena nikaenda kwake kumtembelea akanipa kinywaji kumbe sikujua aliniwekea dawa za usingizi nikalala akaniingilia nyuma tena akiwa ndio ananiingilia kwa mbali nikiwa na kizunguzungu nikahisi maumivu nikawa nalazimisha kuinuka huku sina nguvu na alivyoona nimeshituka akajitoa akaanza kuomba msamaha akasema yeye hawezi kuwa na mwanamke bila kufanya hivyo akasema kazoeshwa na mwanamke wake wa mwanzo ambae alishaachana nae mimi kuona vile nikaamua rasmi kuachana nae nikaona ataniharibia na isitoshe dini inakataza

nikawa naogopa kwakuwa nasikia wanawake wengi wenye mchezo huo wakati wa kuzaa wanapata shida na manesi wanawatukana sana. sasa aunt tatizo ni kwamba baada ya kukutana na mume wangu sikumwambia ukweli kama boyfriend wangua aliyepita aliwahi kunifanyia kitendo hicho ingawa anajua kama niliwahi kuwa na boyfriend kabla yake na kitu kingine aunt mimi sasa hivi nimeolewa na napenda na nahitaji sana kuzaa

lakini naogopa kitu kimoja nikija kuzaa haitojulikana kama niliwahi kufanyiwa hivyo?na pili. watu wengine wanasema kama umezoea ndio unajulikana lakini kwa mara moja au mbili sio rahisi jamani naombeni mnishauri kwani nina wasiwasi nikija kuzaa ikajulikana mume wangua ataniacha na nampenda sana mume wangu na naogopa sana aibu ikijakujulikana hakuna atakae niamini kama sikufanya kwa hiari yangu. please violet naomba msaada pamoja na wadau wote wa blog yako.JE NI KIZAA HAITOJULIKANA.






11 comments:

  1. pole sana kwa yaliyokukuta inawakuta wasicha wengi nikama tu hawajitokizi kusema nivizuri umekuwamuwazi kwani mficha maradhi kilio kitamfichua sijuii ni pepo gani imewaingilia vijana yaani tabia mbaya nanikinyume na maandiko na inamadhara sana tendo hilo ambayo baadhi ya vijana na baadhi ya wazee wanajaribu kualalisha mdogo wangu afadhali umekuwa namsimamo wakukataa hilo tendo lakini mzinifu akajitaidi mpaka akafanikiwa dhambi ni yakwake siku ya mwisho sas nakuja ktk swali lako kwakuwa ulifanya tu mara mbili hukuendelea nafikiri sio mbaya sana huwezi kupata madhara nimbaya kama uliendelea na hiyo tambia ondoa wasiwasi mdogo wangu hutapata shida yeyote

    ReplyDelete
  2. mmh! pole sana jamani, mi nakushauri nenda hospital ukacheki doctor ndio atajua zaidi, lkn umefanya kosa ulivyoanza mausiano na huyo mumeo ungemwambia yaliyo kukuta, kama mimi nishawai kuwekewa madawa kwenye kinywaji soda na mtu alijifanya ananifahamu baada ya hapo sikujitambua, nahisi nilibakwa coz sidiria yangu ilikuwa imegeuzwa siyo kama nilivyovaa, lkn siku na maumivu yeyote niliibiwa hela zangu,mkufu,heleni na pete za dhabu na simu yangu sitosahau nilikuwa na miaka 20,nilienda hospital nilitundikiwa tu drip kutoa ile sumu ya madawa, lkn mpaka sasa sina uhakika kama nilibakwa au la na nilienda kupima ukimwi namshukuru mungu mi ni mzima awafya zote,nilivyoanza tu uhusianao na mchumba wangu nilimsimulia mchumba wangu mkasa wote na hana shida na hilo so nina amani moyoni, so ulitakiwa umsimulie kama anakupenda atakubaliana na yote, ok wewe nenda hospital ukacheki.take care.

    ReplyDelete
  3. pole sana mpendwa ndio mitihani ya duniani hiyo.ninachojua mimi ni kwamba kwa kuwa ulifanya mara n=2 tu na ukaacha kwa muda mrefu bila kuendelea tena hilo sio tatizo na ukiwa mjamzito utajifungua salama bila shida yoyote ila kwa ushauri zaidi unaweza kwenda hospitali na kumuona doctor atakushauri zaidi.kama atakwambia kutakua na tatizo wakati wa kujifungua basi ni vyema ukamwambia mume wako haraka yaliokusibu before yeye japokua utakua umechelewa.Tace care Mama ibra Tata Africa Holdings

    ReplyDelete
  4. pole mpenzi, m nilifikiri unajisikia kuendelea na hiyo laan, wala hautapata madhara yoyote kwa sababu hukuendelea kufanya, wanofanya mchezo mchafuu huu ndo wanamadhara, sikushauri umwambie mumeo, wanaume hawaeleweki unaweza ukamwambia kwa nia njema ukashaangaa nae atataka mjaribu, m nimefanya sana utafiti hilo khs huo mchezo, wanaume wengi waliopo ndoan hawafanyi kwenye ndoa zao lakini huko nje wanafanya, kumwambia mkewe kama anataka huo mchezo wanakuwa waogopa, ukijiloga tu kuazisha utashaa siku nae anataka. usuthubu. na wala usikose amani, wala hutopata matatizo yoyote hiyo sehem itakuwa isharud katika hali yake kma uliingiliwa mara 2 kweli. halfu jikague mwenyew, utajiona kama hizo sehem zimebana au zipo wazi. na usiepende kufikiria hayo yatakukosesha amani, wakti jibu unalo mwenyewe kwa kujichunguza hizo sehemu. muombe sana mungu akutoe katika fikra hizo. nakwambia zitakukosesha amani.

    ReplyDelete
  5. wala haitajulikana babu, mara mbili tu!, watu tumefanya miaka, na tumezaa bila mavi kutoka, na mumeo wala usimwambie, atakutema,

    ReplyDelete
  6. kukushauri tunakokushauri hatumaanishi kuwa sisi ni wazoefu sana, hapana, ila hapa tunachotafuta ni kukusaidia,
    mimi naomba hii iendelee kubaki siri yako na moyo wakotu! mumeo usirogwe ukamwambia, ni kama alivyochangia mdau pale juu, ukisema tu! anaweza nae akakujaribu ili aendelee, au akakuchukia na kukuona malaya, na atalitumia hili kukuumiza wewe, so cha msingi ni kuomba amani, mungu akusaidie, akupe ujasiri na nguvu
    kuhusu kujulikana wakati wa kuzaa, mimi nakwambia hutajulikana hata kidogo, hadi uje ujulikane ni kwamba ushakuwa mzoefu wa muda mrefu sana, lakini kwa mara mbili, tatu, nne, au tano, then umekaa muda wa mwaka mzima bila kuguswa, means pamesharudi katika umbile lake la kawaida, pamefunga, shoga mkund.. ukiachia kila mtu atajua hapa pametema, utanuka wewe, maji yatakuvuja wewe, utapoteza kujiamini, lakini mara mbili tu ! aaaa bwana usiniaibishe, zaa ndugu kwa mapana
    MAMA HILDA, SINGIDA

    ReplyDelete
  7. MSAADA WENU NA KWANGU PLEASEEEEEEEEEE!!!!!!!!!!!1
    jamani dada huyu amenihamasisha sana, mimi ni mzoefu wa kitendo hicho, na natamani sana kuacha, nifanyaje? nilishazoeshwa tena na mume wangu wa ndoa, hadi nimezowea, mwanzo nilikuwa naumia sana, siku hizi siumii hata kidogo, na mimi ndio ninae dai, akinifanya mbele sipati raha hata kidogo, hadi aniingizie nyuma ndio nahisi nimesex
    ila wakati mwingine roho huniuma sana na naapa sitarudia, unakuta kipindi ambacho mimi sitaki, ndie yeye anaweza hata kukasrika hata wiki mbili,
    ili asiende nje inabidi nimpe tu! atulie na mimi maana nampenda sana, jamani naombeni msaada wenu nataka kuwa kama huyu dada, NATAMANI KUACHA, NIFANYAJE NA MIMI??
    violet usibane ujumbe wangu nataka msaada wa mawazo, nahisi nitasaidiwa,
    karibu mwezi wa sita sasa nafanya mchezo huo, yani kila tukifanya mapenzi tu! lazima aipitie nyuma ndio sote tunaridhika, nifanyaje niche ili nisipate madhara, na bado sijazaa? sasa namimi nimeanza kuogopa kuzaa.

    ReplyDelete
  8. pole sana daada nachokushauri usimwambie mumeo na wala usiwe na wasiwasi mm niliwahi kufanya zaidi ya mara mbili nikaacha kwa sababu niliachana na yule bwana sasa nina mtoto na sikupata madhara yoyote na hata mume wangu hajui

    ReplyDelete
  9. Hii mada ni muhimu sana,laah!kumbe ndo maana gay male wanakuwa wengi siku hizi...lo!

    sasa mimi naomba wanaume nao wachangie,ukweli inaonekana hili ni tatizo kubwa,sasa sijui ni tatizo au furaha, maana kuna wengine wanaona raha hasa mchangiaji hapo juu 10:19pm.

    kweli ni sawa kufanywa nyuma jamani kina dada/mama?mimi sidhani kama ni sawa,labda mchangiaji hapo juu atueleze,akipata haja kubwa inakuwaje?je akicheka huko nyuma sikunafunguka?au? maji na harufu?nasikia inakuwa hatari..sasa ukifikia kupata mtoto mwambie doctor wako mapema ili ufanyiwe operation ili mtoto atoke salama,maana kwa hali hiyo siyo kwamba haja kubwa itatoka wakati wa kujifungua...NO! ni hewa itajaa tu nahisi,kwani haja kutoka wakati wakujifungua ni kitu cha kawaida.

    sasa,kweli mchangiaji hapo juu 12:57AM umenifungua,it is true wanaume wanafanya sana haya mambo,mimi kuna mtu alituma msg kwenye simu yangu simjui,akaanza kutukana tu.. from no where,mara nitakufundisha kufanywa nyuma...muhudumie mumeo kwani anapenda sana kufanya nyuma...nilimjibu kibusara tu...kwamba "kufanywa unafanywa wewe..message unanitumia mimi ili iweje?...au ushaanza kuoza nyuma ndo wataka nami nioze...nikamwambia pole we...mpe tu,mimi hajawai kunifanyia hivyo kwani style zetu zinatufikisha tunapopataka ...endelea kunisaidia" sijamsikia tena,ila nilimwambia mume wangu,kama hiyo message ni yakweli basi awe anatumia condom kwani sitaki kufa mapema...kama kawaida yao wanaume alikana kabisa,nikamwambia lisemwalo lipo..

    Ndio maana napenda sana wanaume wachangie hii mada please..hili ni tatizo sana,tena wanaume wengine wapo kwenye ndoa wanafanya sana hii tena kwa wanaume wenzao,mimi nilishaona kaka mmoja anamke wake lakini anamfanya shoga (mwanaume),yani hadi niliwaona one day kwenye foleni (they were kissing)kina dada/mama mliopo kwenye ndoa kuweni makini sana-au mkumbushane kutumia kinga kabisa,msijiamini kuwa my husband is good hawezi...tatizo ni kwamba wanaume wakikutana wanapeana mastory haya na wengi wanapenda kujaribu...

    Dada ulieomba ushauri,usimwambie mumeo naye atataka,tena hasira zote atazimalizia kwa kukufanya nyuma,kama tangu muwe marafiki,wachumba hadi ndoa hujamwambia iweje leo?try to forget it,kama unawasiwasi sana nenda hospital,i think utakuwa poa tu kama wachangiaji wengine walivyochangia.

    All the best!

    ReplyDelete
  10. jamani sijui niwashukuru vipi wapenzi mmenipa amani ya moyo maana nilikuwa sina raha hata kwenye ndoa yangu kwakuwa nilikuwa natamani sana nimzalie mtoto mume wangu lakini nikuwa naogopa sana kutokana na nilivyokuwa nawasikia watu wakiongea kwamba ukizaa unajulikana lakini nashukuru si haba mmeniondoa hofu ahsanteni sana nawapenda wote. ahsante violet kwa kunisaidia pia.

    ReplyDelete
  11. mmh, mi kidume, napenda sana kuangalia porno graphy, na nimejikuta navutika sana na iyo shughuli, ila utakuta ata nikipata demu kumwambia kama napenda mlango wa nyuma inakuwa ngumu sana, naogopa sana asije akaniona wa ajabu. mana mi nna aibu kidogo,anyway kama ina madhara sana nahisi sio fair kumfanyia mwenzako, ila sijapata uhakika kwakweli, coz mimi niliishi mda mrefu london na biliv or not, kuna channel wanashawishi wasichana hasa wa college kufanya analsex, na wanasema ni safe sex! its me nassor11@yahoo.com

    ReplyDelete