Friday, October 22, 2010

TEAM BUILDING - ILIFANYIKA GIRRAFE HOTEL

Tulikuwa na Team Building ya wafanyakazi, namna ya kufanya kazi as a Team, na mambo mengine mazuuuuri sana, ikiwemo michezo na MISOSI, Lo! tulienjoy sana, nilitamani sana kung'ang'ania pale maana lo! kula ni kila baada ya masaa mawili,



Hapa tukiwa ndani ya chumba cha mkutano, tulienjoy sana kiasi kwamba hata wale wa kusinzia hawakusinzia tena, it was fun kiukweli kuanzia wale ma TRAINER wetu, huduma za pale, haswa upande wa msosi we! nilitamani kung'ang'ania huko huko nisirudi,



 Hapo sasa, naona  raha nikiyatizama maji, but lo! kuogelea ni isue, staki hata kujaribu  kuogelea kuna wenyewe bwana, acha tu sisi tupige picha

Mandhari yenyewe ndio kama hivyooo, lo! raha jamani

Kitengo nilichokuwa nikikisuburi kuliko vitengo vyooote ni hiki, yani i wish ningekaa siku tano hivi, but tulilala siku moja tu! unakula kama hutakula tena lo!
Michezo ya maputo, tulicheza sana, tukahisi ni mchezo tu, kumbe kuna somo ndani yake, TUMEENJOY SANA
(Nawe enjoy kupitia this pictures)
I LOVE YOUUUUUUU





3 comments:

  1. dada mmependeza. Ila naomba kukuuliza. Nimeona umevaa kikuku mguuni. Mimi ni mdada mwenye kazi kubwa (respectable) ila kwa kweli napenda sana kikuku. Tatizo langu naogopa watu watanionaje kwani nasikia kina tafsiri mbaya. Nisaidie. Yaani natamani ninunue kesho though si kwa maana za watu ni urembo tu. Nishaurini wadau.

    ReplyDelete
  2. Asante sana mdau hapo juu, kusema ukweli mimi huwa siangalii watu wanasema nini, coz watu wanawezatamka lolote, na hivi maneno hayalipiwi VAT, basi wanaweza kusema chochote kikakuumiza, so huwa naangalia mimi napenda nini? nikivaa vipi ndio nakuwa free, nafsi yangu ikikubali tu! basi nitafanya hivyo, kwanini niidhurumu nafsi yangu?
    Mimi huchukulia kikuku kama pambo lingine, kama cheni shingoni, bangili mkononi, heleni sikioni, pete kidoleni, hali kadhalika kikuku mguuni, na siamini wanaosema kikuku kina mguu wa kuvalia, mimi huvaa mguu wowote ninaojisikia, wale wa kusema husema weeee, wanaonuna wananunaaa, wanaoona kawaida wanaona hivyo, siku zinakwenda hadi leo,
    USHAURI
    Mpendwa wangu, dunia ya sasa mtu kukupa raha ni adimu sana, RAHA JIPE MWENYEWE, na pia jikubali kwanza ili watu wakukubali, ukianza kujipa mashaka basi utaishi kwa shida, coz hata watu wasipokutazama utaona kama wamekutazama, basi hata ukikivaa kikuku hutakuwa free utatamani ukiona watu ukimbie ukajifiche, sasa inakuwa haina maana,
    DO NOT LISTERN WHAT PEOPLE ARE SAYING, Coz some ot them watakuumiza tu!
    i love youuuuu

    ReplyDelete