Wednesday, November 9, 2011

MUME WANGU ANATAKA PENZI KWA MTOTO WANGU WA KUMZAA MWENYEWE, NIFANYAJE?

dada Violet nahitaji msaada nina mume wangu nampenda ila kwa sasa sijui kama naye ananipenda ama vipi, nasema hivi kutokanana na vitu vyake,

 iko hivi mimi kabla ya kuwa na huyu mwanaume nilikuwa na mtoto mmoja wa kike kwa sasa ana miaka kumi na sita, na yeye tumefanikiwa kupata watoto wawili wakiume tatizo ni kwamba huyu bwana ni mlevi, mchafu hapendi kuoga yeye akioga asubuhi  ndio imetoka anarudi analala tu na jasho la pombe  na akiwa katika hali hiyo anataka kusex mimi kiukweli nashindwa kusex najisikia kinyaa,



 tabia yake nyingine na kuwalazimisha wasichana wa kazi wafanye naye mapenzi nimepata malalamiko kama manne hivi nikimwambia anakuwa mkali, sasa kubwa kuliko yote juzi karudi kalewa anafunguo yake kaingia ndani kaenda kugonga kwenye chumba cha watoto wa kike anamwambia yule binti yangu umekuwa sasa eti anataka wasex na akawa anamlazimisha kwa nguvu,

binti akakimbia akaenda kwa housegirl naye akakimbia mimi hapo nimelala maana ilikuwa kitu saa kumi usiku hivi, kesho yake mtoto wangu akaniambia na akasema mama mimi sitaki kuishi hapa tena nimechoka na tabia za baba hata dada

dada (jina nalihifadhi) aliyeondoka, aliondoka kwa ajili ya baba, maana alikuwa anamlazimisha kufanya mapenzi nikashtuka kumbe hata mtoto ana hadithi zake.

nifanyeje wadau niendelee naye au naona nimechoka nahitaji kuwa peke yangu kwa kweli sioni ninachopata kwa bwana huyu zaidi ya mawazo,




8 comments:

  1. nchi za wenzetu,huyo bwana angetiwa ndani.hee wee mama wee,baada ya issue hiyo unasema unampenda mume wako?mimi mume wangu amtake mwanangu huyo mimi na yeye,mapenzi yanakuwa mwisho.huyo mtoto kimbilio lake ni kwako.ukiwa upande wa huyo bwana,huyo mtoto atakuwa mnyonge.leo hii ukishazeeka,huyo mtoto akikuchukia utamlaumu?na kwa nini huyo bwana awe kutwa analewa tu?sababu gani inamfanya awe mlevi hivyo?

    ReplyDelete
  2. Pole sana bibie.Mimi ni mwanaume, kiukweli nikuambie kuwa mtu mlevi ni kama mgonjwa wa akili maana hawezi kujitambua kabisa na ndio maana mumeo anaparamia hao mabinti. Akili huwa inamtoka kabisa.ndio maana akiwa hajalewa hawezi kufanya hivyo.

    Dawa ni kuacha pombe kama angekubali, vinginevyo ataendelea kuharibika zaidi na zaidi na si ajabu huko nje anatomba hata bila kuchukua tahadhali yoyote.Mimi nadhani ukae naye ongea naye kama kuna watu wanaweza kuwasaidia.kama haiwezekani kwa kweli ndoa hiyo haitafaa kabisa maana ni balaa kama baba anavamia watoto wa kike utakaa na nani sasa.hata hao wa kiume atawavamia tu iwapo wa kike watahama hiyo nyumba, maana waswahili husema "Mbaazi akikosa maua husingizia Jua" Vinginevyo kimbia kabla ya hatari zaidi.

    ReplyDelete
  3. achana na huyo baba, anakupotezea muda tu! mtu gani asie hata na aibu jamani, hadi kwa mtoto wa kufikia anataka penzi, hata kama ni UCHU, HUO WA KWAKE UMEKUBUHU, MWACHE NA UMALAYA WAKE

    ReplyDelete
  4. Dada kimbia kaanze maisha yako na watoto,huyo atakuja kukubaka hata wewe mwenyewe,huyo mwanaume ni mpuuzi kama hawezi hata kumuheshimu mtoto wako mwishowe ambake mama yako mzazi.

    ReplyDelete
  5. pole kwa kuendelea kukaa tu! mh! binadamu wengine sijui mna mioyo ya paka, yani lijitu lihuni hivyo bado upo nalo nyumbani, na unataka ushauri, mmi kwa upeo wangu mdogo, nafikiri kuna vitu ambavyo wala havihitaji ushauri kabisa,

    ReplyDelete
  6. MH! HAKUFAI DADA, HATUNA CHA KUKUSHAURI ZAIDI YA KUANZA MAISHA YA PEKE YAKO, NA KWELI NAKUAMBIA UKIENDELEA KUKAA HAPO JIANDAE KUPOKEA NA UKIMWI

    ReplyDelete
  7. yaaani kweli unauliza kama uendelee kukaa? mumeo atatakaje kulala na mwanao alafu unauliza eti niendelee kukaa nae?

    huyo sio mwanaume ni mnyama tena mnyama pori kabisa.. ingekuwa mimi ningemchoma na mafuta ya taa akiwa amelala acha nikafie jela

    chukua kinachokuhusu nenda kaanze maish yako mbele ya safari na sahau kabisa huyo mwanaume sio binadamu labda katumwa na LUSIFA... hata kama umezaa nae achana nae kabisa dada maana mwisho utasikia anataka kusex na mama yako mzazi

    ReplyDelete
  8. mnh pole sana aunt,huyo si mwanaume wakuendelea kukaa nae ni mshenzi tena mbwa,cha muhimu ni kudai talaka yako na kuondoka,inshalah MUNGU atakua pamoja nawe kwani huachika kwa kupenda bali kwa matatizo makubwa yaliyokupata.

    ReplyDelete