Saturday, September 17, 2011

NAUMWA SEHEMU ZA SIRI, NIMETUMIA DAWA SIJAPONA NIPENI USHAURI

Pole na kazi dada yangu. Mimi ni mpenzi sana wa kusoma hii blog yako na nimefaidika na mengi juu ya hii blog yako. TATIZO langu ni kwamba nilipata infection/ maambukizi nadhani ni ya ugonjwa wa zinaa kutoka kwa mchumba niliokuwa nikamwamini sana

lakini kuna Siku baada ya kusex nae niliona kama maziwa yananitoka kwenye uume wangu hiyo ni kabla ya kukojoa. Nilienda hospitali siku hyo hyo. Docta aliniambia ni kisonono. nilitumia dawa ikaacha but ikarudia tena. Nilienda tena hospitali wakanifanyia culture and sensitivity wakasema hamna wakanitoa damu wakasema pia hamna lakini bdo tatizo lipo tu nikitumia dawa linaacha baadae linarudia na kwa sasa ule ute unazidi kuwa mzito inakuwa kama chai ya maziwa hivi au cream ya njano isiyo kolea.

Nahitaji msaada wa haraka sana naomba hta mtu nipe namba yke kama anaexperience na hicho kitu. au labda kuna doctor atakaeweza kunitibu, hali hii imeninyima raha sana. hadi sasa, yani sijielewi, Huyo msichana nilishatengana
nae siku ileile nimechanganykiwa plz nisadien huu mwez wa 3 sasa




5 comments:

  1. Kaka pole sana, mi ninavyojua ugonjwa wowote wa zinaa kwa mwanaume inachukua siku nane kujitambua kama unao... yawezekana ulishaupata kabla ya hiyo siku mlivyokutana au hata wewe mwenyewe uliruka nje na kukutana na mwanamke mwingine kabla ya huyo mchumba wako, lakini kama una uhakika ujakutana na mtu mwingine kimwili isipokuwa huyo mchumba wako, basi alikuambukiza wiki moja kabla ya kukutana nae tena, na kwa upande wa wanawake inakuwaga ngumu sana kujitambua haraka akishaambukizwa ugonjwa wowote wa zinaa na ndio mana utakuta mpaka mwingine ananuka na kutoa majimaji sehemu za siri ndio anagundua kuwa hayuka katika hali ya kawaida... so kama wewe ni mwaminifu na una mpenzi mmoja tu ujue yeye ndo ameruka nje akaleta maambukizi hayo... kwa ushauri wangu unaweza kumwona Gynenocologist(dactari wa kina mama) wanaweza wakakusaidia mana wao pia wanahusika na magonjwa kama hayo, na ndio maana mwanamke akiumwa ugonjwa wowote wa zinaa akienda kwa dactari wake wa kike anamwambia kamlete na mumeo au mpenzi wako ili muweze kutibiwa wote mpate kupona na kuzuia maambukizi endelezi... so kama uko DAR nakushauri uende agakhan hospital jaribu kumwona DR. SHAFIQ kwa ushauri au uende Tumaini hospital mwone DR. KAPONA au nampa dada violet namba yangu atakupa alafu ujaribu kunitafuta them nitakusadia kumpata mtu anayeweza kukusaidia.

    ReplyDelete
  2. pole saaana una UDS Urethral Discharge Syndrome inatibika kaka Hosp wala usiwe na presha pia hujasema kama ulienda Hosp na demu wako ili mtitibiwe wote maana ukijitibu mwenyewe kaka havisaidii hapo ni wewe na yule na yuleeeeee pole saana Fika Hosp tu na siha itakwisha 45k

    ReplyDelete
  3. pole kaka, nenda agakhan au regency hospital, onana na dr mgonda, au huyo ulieelekezwa hapo juu, mungu atakusaidia utapona,

    ReplyDelete
  4. asanteni wadau, kwa kumshauri kaka yetu, ila wewe ulieshauri hapo juu kabisa, naomba uniutumie namba zako kwenye email yangu violet.gerald@yahoo.com ili nimpatie huyu kaka muweze kuwasiliana, tuone jinsi utakavyomsaidia, ameinsist sana ufanye hivyo,
    asante kwa ushirikiano wako

    ReplyDelete
  5. asante dada violet, kwa blogu yako ya kutusaidia, kaka, wahi hospitali mapema, tatizo lako linatibika

    ReplyDelete