Tuesday, August 24, 2010

RAMADHAN KAREEM WADAU

Nilikuwa na Likizo mbili:-
1 Masomo/Mitihani
2 Pia likizo yangu ya kawaida kwa kila mfanyakazi
Sasa inakaribia ukingoni kabisa, nitarudi FULL.

1 comment:

  1. Wengine walikuwa wamesinzia
    Niko kwenye daladala, watu wametulia kila mtu akitafakari mambo yake. Mara kaibuka abiria mmoja akavunja ukimya akauliza." WaTanzania wenzangu naomba kuuliza swali". Abiria wote tukageuka kumwangalia. akajitolea dada mmoja akamjibu, "uliza tu baba" unajua aliuliza swali gani? ha ha haaaaa!!

    Akauliza:- Jamani mie binti yangu anaolewa tarehe 31 siku ya uchaguzi, sasa aolewe au asiolewe?Maana polisi wasije wakatukamata kwa kufanya sherehe siku ya uchaguzi.

    Haya haya mdada nadhani likizo imekwisha karibu tena katika mpambano wa kujenaga taifa na kuelimisha jamii.Sasa basi mdata nirushie hiki kibom maana nilikipatia kwenye daladala.Kiukweli ukipanda kwenye dalalada utakutana na vihoja.Kuna baba mmoja alisema ndugu zangu nina swali.Akajitokeza Bidada mmoja akasema uliza baba.Akasema jamani nina binti yangu anaolewa siku ya uchaguzi aolewe au asiolewe?Pakazuka malumbano miongoni mwa abiria, wengine wakisema aolewe na wengine wakisema asiolewe kwani watakamatwa kwa kufanya sherehe siku ya uchaguzi. Mpaka nateremka kwenye daladala bado malumbano yalikuwa yanaendelea kama ujuavyo kwenye daladala kuna wapiga doma kwa sana. Kaazi kwelikweli!!!
    Habari hii nimetumiwa na msomaji wa Maisha na Mafanikio aishiye jijini Dar es Salaam.

    ReplyDelete