Monday, July 30, 2012

ANATAFUTA MUME,,,,,


mimi ni mdada mwenye umri wa miaka 29 .nimeokoka nasali kanisa la fpct .tatizo langu sijapata mume aliyeokoka kila ninaye mpata hajaokoka na mimi natamani sana kuolewa na mwanamme aliyeokoka na mwenye hofu ya mungu lakini mapaka sasa sijapata hii hali inanitesa sana moyo wangu maana hata mdogo wangu wa mwisho amepata mimi bado.nimechoka kuwa pekee yangu natamani kuwa na familia na kuwa na watoto.nimefurahi sana kukuona blog yako Mungu akubariki kwa kuanzisha blog hii .




Thursday, July 26, 2012

ANATAFUTA MCHUMBA MWENYE HIZO SIFA JAMANI.......... (Hii picha sio yeye, ila ni kuonyesha msisito wa kijana anataka mke kweli.....

Habari yako dada. kwanza kabisa nakupongeza kwa kazi nzuri unayoifanya ya kutoa ushauri, na pili napenda kuomba msaada wako, uniwekee hii post yangu ya kutafuta
mchumba kwenye blogu yako. Na maelezo yangu ni kama ifuatavyo;

Naitwa Salim Athuman, umri wangu ni 27, kwa imani ni Muislamu na kwa sasa ninaishi DSM.Nahitafuta msichana mwenye umri kati ya 22 hadi 25 na sifa kubwa awe Muislam, mpole na mwenye kujiheshimu na kujistiri(Mwenye kuvaa mavazi ya heshima). Itakuwa vizuri awe mweupe/ maji ya kunde, mrefu kiasi na mnene kiasi na mwenye elimu at least diploma. Dhumuni kubwa ni kuwa mchumba wangu kwa sasa na hatimaye Mungu akipenda tuje kufunga ndoa na kuishi pamoja hapo baadae. Kiukweli nimevumilia sana kuwa mwenyewe kwa kipindi chote nilichokuwa nasoma, japokuwa kwa sasa bado naendelea na elimu zaidi ila nahitaji na mimi kuwa na mwenza wangu. Tafadhali kama upo tayari kuwa nami naomba tuwasiliane.


kama uko serious niinbox mimi
violet.gerald@yahoo.com ili nikupe mawasiliano yake