Hello
miss violet
Nimekua
nikifuatilia sana matukio yenu na jinsi watu wanavyotoa uashauri nimeguswaa
maana na me nina langu lanitatiza na sijui nifanyaje yaaani sina jinsi ya
kufikiria tena.
Nilikua na bwana ambae alikua ananipenda sana
ila mimi sikuampenda kiiivyo nkaamua kuachana nae maana ntamuumiza tu maana
sikua muaminifu kwake na nkawa najisikia vibaya, kwa ilo nkaamua kumuacha
aendelee na maisha yake.
Nilipoachana
nae nkapata mkaka mwingine ambae kanionesha maisha ambayo sijawai kua nayo ninampenda
sana uyu kaka na yeye ananipenda saaana ila ni anawivu na hasira mbayaa ila
sababu namuelewa namchukulia kama alivyo najua jinsi ya kumuhandle kama
anahasira ilaaa tatizo kubwa ni lililopo ni DINI,
Yeye ni
muislam na mimi ni mkristo, ndugu zangu washaanza
kunijia juu kua hawataki niolewe na muislam, kifupi hawataki mausiano yangu nae
na me nampenda sana jamani nina furaha kuwa nae, tuna amani na niko huru saaana kwake!
Mbaya zaidi mama yangu anasema anatambua
ndoa moja tu ya kikristo nyingine hazitambui nisaidieni jamani
nifanyaje?? Na hatuko tayari kuachana!!!