Naomba ushauri kwako dada violet na wadau wengine, Mimi ni mke halali wa mume
mmoja na watoto wawili, ndoa yetu ina miaka kumi sasa, ugomvi huwa haukosekani ndani ya nyumba,
lakin naona kwangu imezidi, mume wangu amekuwa na dharau kupita kiasi, hanijali
mimi wala familia (watoto).. yani upendo
wake ni wa kubeep
Ananichosha tunapokuwa
kitandani, yani imefika kipindi inapita
hata wiki tatu au nne bila kugusana kimwili, na kama nikihitaji inachukuwa muda sana hadi kukamilisha tendo,
hisia zake zinakuwa mbali sana na mimi, yani in short simuelewi huyu mwanaume…
watu wamenishauri nimdharau tu! Lakini mimi dharau siwezi, naumia mno jamani,
bora ukose pesa uwe na amani, kuliko uwe na pesa ukose amani, nishaurini
wapendwa wangu