Mume wangu hanishirikishi kwenye maamuzi ya familia, naona tu mabadiliko yanafanyika ndani, lakini siambiwi chochote, kazi yangu kupokea tu! Sasa nimesikia tetesi kuwa anajenga huko kwao, lakini mimi mkewe wa ndoa sijui chochote, cha ajabu mama yake mzazi ndio anajua kila kitu, na huyu ni mume wangu wa ndoa, tuna miaka nane kwenye ndoa yetu, ukimuuliza anakuwa mkali sana, tumezaa watoto wawili mpaka sasa.
Mimi nina kazi nzuri tu na nina mshahara mkubwa Ambao naweza kufanya vitu vya maana, nilivyokwisha vifanya hadi sasa nimejenga nyumba 2, moja ndio hii tunayoishi na mume wangu, sasa mwenzangu ndio kanibadilikia sana, hata simuelewi, je namimi nianze kufanya mambo kivyangu??? Lakini naona kushare Ideas ni nzuri zaid, wadau nisaidieni naona nimetegwa sana, na pia kwanini asinihusishe mimi mkewe?? Kajenga baa kubwa tu kwao! Lakini mimi Nimejua nilipokwenda kwenye msiba wa kaka yake, nilipomuuliza ilikuwa ugomvi sana.na hadi sasa hata sielewi nilichomkosea