Wednesday, October 31, 2012

EWE MWANAMKE, JIANDAE KUKUTANA NA WANAWAKE WENZIO TAREHE 1 DEC 2012,





Kutakuwa na chakula cha usiku, tutacheza, tutakul, Tutakunywa, tutapata mafunzo mazuri kabisa kwa ajili ya kudumisha furaha katika suala zima la mahusiano ya kimapenzi, sherehe itabase sana kwenye masuala ya BEDROOM,
Kivazi chetu siku hiyo kitakuwa ni black and gold kwa upande wa rangi, stay tuned, muda sio mrefu nitawatajia mahali itakaapofanyika,,ni nzuri sana kukutana na wenzio, kubadilishana mawazo, kushare challenges ambazo tunakutana nazo katika maisha yetu ya kila siku, hatimae kupata majibu yaliyo sahihi... vyote hivyo utavipata kwa shiling 30,000/= yako tu, unatuma kwenda namba 0757643422 M-PESA, na TIGO PESA kwa namba 0719-178 228,, hii sio ya kukosa,, karibuni

Thursday, October 25, 2012

NIMEMJUA MWANAMKE ANAETEMBEA NA MUME WANGU,, NIMEUMIA SANAAA, NAOMBENI USHAURI WENU



Habari violet,
Naombeni msaada wa maawazo yenu, nimegundua kuna mwanamke anatembea na mume wangu, mume wangu alikataaaaaa kwa mara ya kwanza, lakini baada ya kufatilllia na kuchunguza kwa muda mrefu nikaja kuhakikisha ni kweli kabisa, mwanamke anaomba msamaha kwamba wataachana na hatorudia tenaa, na mume wangu pia anasema hatorudiaa,

Nimeumia sana mwenzenu, nimeumia kupita kias, kwakuwa nilimpenda, nilimheshimu, nilimjali sana mume wangu, nilikuwa teyari kumuachia yeye kila kilicho changu, nilimsikiliza sana, sikutegemea kama atakuja kunitenda hivi, imekia kipindi najuta kwanini niliolewa nay eye,  sikutegemea kabisa kutokana na muonekano alio nao,,, details zoote za huyo mwanamke wake niko nazo, niliomba niprintiwe kupitia mitandao ya simu wanayotumia, niko nazo mkononi, staki kuamini, ninalia kama mtoto mdogo, ni bora niibiwe pesa nitatafuta, kuliko kuibiwa penzi,, nitalipata wapi,,
Nimechanganyikiwa, nataka kuondoka kwenda kwetu nikapumzike, nimwache kwanza, maana kila nikimuona Napata hasira natamani kumkaba kabisa, nimemchukia mno,,, sina amani ya kuwa nay eye, hali hii hadi lini?? Nifanyaje?

Monday, October 15, 2012

NILIWAMISSSSSSSSSSS

weekend yangu ilikuwa kama hivyo,,, tulikwua lion hotel(sinza). kulikuwa na party ya kina dada tu, kukutana, kubadilishana mawazo, kuondoa stress za maisha,,, na mwisho ni kufahamiana,,, ilipendeza sana, jiandaeni nitawaletea picha....
\