Monday, September 26, 2011

HAYA, KWA WALE WALIOHITAJI VITU NINAVYOTUMIA KATIKA KUJAZA,KUKUZA NA KUPENDEZESHA NYWELE ZANGU

Kwa leo ninawaambia ni nini na tumia, ila nitaandaa picha za hivyo vitu pia ili niwatumie wiki ijayo,
Dawa ninayotumia ni Olive Oil,  zipo za aina tatu, na zote ni bidhaa za olive, na ambayo huwa naitumia sana ni ile yenye picha ya mtoto kwenye box, ambayo ndani yake ina kikopo kidogo cha steaming


Natumia Avocado shampoo, ni nzuri sana, lakini hata kama utaikosa kwenye haya masalon yetu waweza tumia shampoo yeyote ile,  mradi nywele zioshwe na zitakate, na pia tutumie conditioner, baada ya kuosha na shampoo, conditioner inasaidia sana kulainisha nywele na kuzuia zisikatike wakati wa kuchana, ni muhimu sana kuwa nayo, kama kwenye masalon yetu hakuna, basi nunua kifumu au kopo lako then unakuwa ukienda salon unamimina kidogo unakwenda nayo,


Huwa natumia mayonise steaming,  hii pia ziko za aina mbili, kuna le kubwa kabisa ambayo ni white cream, na kuna kubwa kias ambayo ni dark cream, I mean cream iliyokolesa sanaaaaa,
Sasa hii iliyo koleza sana ndio huwa natumia, na ninaitumia kila wiki, yani kila juma pili lazima nifanye steaming
                                      
Baada ya kuosha nywele zangu toka kwenye steamer kabla ya kupaka pinki lotion na kuanza kuseti huwa napaka kwenye ngozi ile steaming iliyopo ndani ya dawa,  naipaka kwenye ngozi tu! Kisha inachanganywa, halafu ndio unapaka pinki lotion kiasi tu(hii haioshwi, unasetia
 

Baada ya nywele kukakuka huwa natumia Blue magic chafu, wenyewe wauzaji wanaita blue magic ya chenga, inapakwa kwenye ngozi, na juu, kama ukikosa tumia hata Venus, but  blue magic ni nzuri zaidi naona inajaza sana nywele, inalainisha, na kuzifanya zikae wiki nzima zikishine, coz mimi huwa nikipaka jumapili sipaki tena hadi jumapil ingine na nywele huendelea kulegea na kubaki katika mvuto wake

HIVYO NDIO VITU NINAVYOTUMIA KICHWANI KWANGU

ADDITION

1.     Usisubiri harusi au sikukuu ndio uende salon, jitahidi kila wiki, au kama utashindwa basi atleast mara mbili au tatu kwa mwezi

2.     Kata ncha za nywele zako kidogo kila baada ya miezi miwili unapotoka kuretouch

3.     Usisuke nywele siku chache baada ya kuretouch, utazikata,  acha ziotee kwanza ndio usuke,

4.     Usifumue nywele kama unagombana, fumua taratiibu, kama umesikuka kimasai basi ikibidi chambua nywele moja moja kwa kutumia sindano,

5.     Usipende sana kutumia loterbody au jerry, hii inakata sana nywele labda kuwe na sababu maalum ya kufanya hivyo, lakini, mh! Sishauri sana
6.     Kwa wale wapenda rangirangi kama mimi, unapoweka breach, usifikishe kwenye ngozi, (shina la nywele) breach inapakwa kwa juu tu!

7.     Pia wale wa kutong, ni nzuri sana kutong kwa kutumia rolas au mabomba ya mipapai au mirija ya juice, lakini kutong kwa kutumia mashine, sio kuzuri sna  sababu mashine inaunguza nywele, 

8.     Usiwejiweke dawa mwenyewe kama sio mtaalamu au usimpe mtu asielewa namna ya kuweka dawa , atafanya zikatike, that’s  whay unashauriwa kwenda salon,


Kuna uwekaji wa aina mbili,
a)     Kwa wenye nywele nyingi na kavu hadi juu, unaporetouch anza chini, then katika kuchanganya apake hadi juu ili kulainisha zile za juu, 


b)    Kwa wale wenye nywele chache, na laini, unaporetouch usifikishe dawa juu utazimaliza, weka dawa chini tu! Kule kuliko otea, na kama ni chache halafu kavu, basi rambisha kidogo kwa juu dakika kumi au 15 kabla ya kuosha,
c)     Jitahidi unaporetouch usiwe na Mba nyingi kichwani, maana zinasababisha kuungua sana na kung’oka nywele kutokana na majeraha,

PAMOJA NA VYOTE HIVYO, NYWELE ZINAHITAJI USAFI SANA, ILI ZIPATE NAFASI YA KUKUA VIZURI, HATA KAMA UMESUKA UNAWEZA KWENDA SALON UKAOSHA NA KUKAUSHA, HIZO NYWELE ULIZOSUKA
HIVI  NDIVYO NINAVYOFANYA MIMI KWENYE NYWELE ZANGU, BUT KAMA NILIVYOWAAHIDI WIKI IJAYO NITAWATUMIA PICHA YA HIVYO NINAVYOTUMIA ILI UVIONE,

Friday, September 23, 2011

WE WISH YOU A NICE WEEK END

Me, my lovely Twins (Tymon & Trace)
We are wishing you a happy weekend
We love you all

Saturday, September 17, 2011

NAUMWA SEHEMU ZA SIRI, NIMETUMIA DAWA SIJAPONA NIPENI USHAURI

Pole na kazi dada yangu. Mimi ni mpenzi sana wa kusoma hii blog yako na nimefaidika na mengi juu ya hii blog yako. TATIZO langu ni kwamba nilipata infection/ maambukizi nadhani ni ya ugonjwa wa zinaa kutoka kwa mchumba niliokuwa nikamwamini sana

lakini kuna Siku baada ya kusex nae niliona kama maziwa yananitoka kwenye uume wangu hiyo ni kabla ya kukojoa. Nilienda hospitali siku hyo hyo. Docta aliniambia ni kisonono. nilitumia dawa ikaacha but ikarudia tena. Nilienda tena hospitali wakanifanyia culture and sensitivity wakasema hamna wakanitoa damu wakasema pia hamna lakini bdo tatizo lipo tu nikitumia dawa linaacha baadae linarudia na kwa sasa ule ute unazidi kuwa mzito inakuwa kama chai ya maziwa hivi au cream ya njano isiyo kolea.

Nahitaji msaada wa haraka sana naomba hta mtu nipe namba yke kama anaexperience na hicho kitu. au labda kuna doctor atakaeweza kunitibu, hali hii imeninyima raha sana. hadi sasa, yani sijielewi, Huyo msichana nilishatengana
nae siku ileile nimechanganykiwa plz nisadien huu mwez wa 3 sasa




Sunday, September 11, 2011

MZAZI, MUDA GANI UNAKAA NA WATOTO WAKO NYUMBANI??




Swali hili ni la msingi sana kwa mzazi anaejali mtoto wake, wazazi tumekuwa busy mno, kiasi kwamba tunawasahau watoto wetu kabisa, kuna kipindi kiliwahi kunikuta mimi nikitoka saa 12 naenda kazini naacha wamelala, nikitoka kazini naenda chuo, narudi home saa mbili na nusu au saa tatu nakuta wamelala, yani ilinipa wakati mgumu sana,sasa naamini hii inatokea na kwa wengine pia kutokana na shughuri tulizonazo, muda umekuwa upo pale pale ila majukumu ndio yametuzidi


Nawakumbusha tu! Wazazi wenzangu siku tunazokuwa na muda, lets say ni weekend, tukumbuke kuwa karibu nao sana, tuwadadisi kiundani sana kujua mawazo yao, michezo yao na hata mahusiano nao na dada zao (mahousegilr) tuangalie homework zao, tukague madaftari yao, kwa kufanya hivi tutagundua vitu vingi sana, ambavyo wamejitahidi, au wanahitaji msaada zaidi


 nilichogundua kwao hasa kwa hiki kipindi ambacho niko rikizo ni kwamba wanapenda sana kila kitu niwafanyie mimi, mfano wakiamka tu! wanakuja chumbani kwangu moja kwa moja, na kunitaka mimi niwaandae, na sio dada tena, so namwambia dada endela na kazi zingine, ngoja niwahudumie mimi. basi wanafurahi sana, nikimaliza kuwapa chai, wananiambia mama utupeleke hadi shuleni kwetu, kwakuwa sio mbali na nyumbani, basi nawasindikiza wananipa mabegi yao niwabee, yani wanaenjoy kupita kiasi, hata kwa kuwa namimi kwa dakika chache tu!


Tusiwaamini sana wadada wa kazi, coz wao sio wazazi, ni wachache sana wanaofanya exactly like mother, but mmmmm… bado kama mzazi especially mama, unahitaji kuwa karibu na mtoto sana, ukiwa na mtoto ambae sio muoga atakufanya ujue vitu vingi vinavyojiri nyumbani wakati haupo, mfano tracy wangu, kila kinachojiri nyumbani hasahau,  ukirudi tu! Kama akiwa macho anakuelezea, naanza kumfanya rafiki yangu tangu akiwa mdogo, ili asiniogope bali aniheshimu  na awe wazi kwangu, maana kumkaripia sana kunampotezea confidence kabisa, anahisi kila atakachofanya atafokewa, so nivizur sana kusoma tabia za watoto wetu INAPOBIDI KUWA MKALI, KASIRIKA NA MTOTO AJUE NIMEMUUDHI MAMA AMEKASIRIKA, LAKINI ISIWE NONGWA, KILA SAA UNAKASIRIKA MTOTO ATAKUCHUKIA


Weekend hii nimekumbuka kugusia watoto, naona limekuwa ni tatizo kwa baadhi ya wamama,  siku ukipata nafasi, andaa chakula cha watoto wako wewe mama, dada nae apumzike, angalia walipohifadhiwa nguo zao za kushindia, angaliwa walipolala kila siku, kagua kabla hujalala,  je vyandarua vyao ni salama? Kagua kucha zao kila weekend, kata ziwe fupi, yani atleast uwe na hata nusu siku kwa ajili yao,



Kweli nawaambia mtoto hujiskia fahari sana anapokuwa na wazazi wake, baba au mama au wote, japo watoto wengi wameegemea sana kwa mama, hawataki utoke, ukitembea nao wanajiskia raha sana,

 
KWENU WAZAZI NATAMBUWA MNAFAHAMU WAJIBU WENU KWA WATOTO,  BUT WENGI WENU MNAJISAHAU SANA KUTOKANA NA SHUGHURI ZA KILA SIKU, NAJARIBU KUWAKUMBUSHA TU,  JINSI TUNAVYOLEA WATOTO WETU, NDIVYO WATAKAVYOKUWA KUWA,

KIKUBWA NA CHA MSINGI, PAMOJA NA UBUSY TULIONAO TUSISAHAU KUWAOMBEA KILA SIKU, ILI MUNGU AENDELEE KUWALINDA KWA KILA KITU

NAWADORISHIA NYWELE ZANGU


MWANAMKE NYWELE BWANA, MAWEAVING KILA MARA YANACHOSHA NA JOTO HILI LA DAR

SIO WEAVING WALA NINI

Add caption

KWA NYUMA

NIKO NA AUNT WANGU CAREEN, NATAMANIA KWELI KAKUWE ILI NIKASUKE


Friday, September 9, 2011

MTOTO WA MUME WANGU ANANIFANYA NITAMANI KUIKIMBIA NYUMBA YANGU- NISAIDIENI

Mimi ni mama niliolewa miaka mingi iliyopita, nilimkuta mume wangu ana mtoto mmoja ambae ni mdogo sana, mama yake alikuwa amefariki ndio nikaolewa mimi,
Nilimlea Yule mtoto kama wa kwangu mwenyewe, nilimuhudumia na kumpa mapenzi yote ya mama, nami mungu akanijalia nikapata mtoto mmoja wa kiume,

tatizo ni kwamba huyu mtoto wa mume wanguameshakuwa  yuko form four sasa hivi,lakini nilianza kumlea toka akiwa na miaka mitano,
Juzijuzi hapa nilihisi ni mjamzito, nikampima nikakuta ni kweli, iliniuma sana kwakuwa bado ni bint mdogo istoshe hata shule bado hajamaliza, nilimsema sana, cha ajabu baba yake toka kipindi hicho hadi leo hii hajasema chochote na binti yake kuhusu huo ujauzito, mbaya zaidi anamtetea kwa kila kitu kias kwamba Yule mtoto anaweza kunijibu vile anavyotaka, nikijaribu kumuonya anakuja juu sana, na baba yake anamtetea,

Natamani hata kuikimbia nyumba yangu, maana sielewi itakuwa hivi hadi lini, mtoto amekuwa mjeuri kupita maelezo, tena anasema kwanini wewe unifatilie fatilie wakati baba yangu anajua na hajasema lolote juu ya hili, wewe ndio una uchungu sana???
Sasa jamani mimi kama mimi sijui nifanye nini kabisa, tunaishi kama mtu na mke mwenzie yani ukikuta ananijibisha as if ni mdogo wake, naombeni  ushauri, nifanye nini mwenzenu??