Mashost wamechachamaa jamani na waume za watu, kuweni makini nao, haya mambo ya shemeji yako huyu!, chukuwa namba yake hii! sijui leo tunatoka twende utupe company, mh! shauri yenu,
soma hii ya huyu dada! imenigusa sana
(ni ndefu mno, but nimejitahidi kuedit na kubakisha points tu!)
Habari yako dada,
Nimepewa jina la blog hii na Arafa, anasema mlisoma nae, nahitaji sana msaada wako dada yangu, mimi nilikuwa na kijana mmoja tuliependana kupita maelezo tulikutana chuo cha ufundi, mimi nilikuwa nasoma kozi ingine na yeye ingine, baada ya kumaliza akaamua kunichukuwa na kuishi na mimi, tumeishi nae kwa muda wa miaka mitatu kama mke na mume japo mwenzangu umri wake umeenda kidogo, tumefanikiwa kujenga nyumba mbili, baa mbili, yani hatukuwa na maisha ya shida, na nimezaanae mtoto mmoja,
Niliwahi mtambulisha rafiki yangu kwa mume wangu, hadi sasa naandika ujumbe huu ni miezi mitano nimetengana na mume wangu, alinifukuza kwake, nikamuuliza kosa langu ni nini? Akasema eti dini hazifanani yeye mkristo na mimi muislam, nikamuuliza sababu ni hiyo tu?? Hukuliona hili tokea mwanzo hadi kunichukuwa na kunizalisha? badae Nikakubali mimi kubadili dini ili niendelee kuwa nae, sikufichi violet huyu ndie mwanaume wangu wa kwanza tangu nizaliwe, wazazi walinikatalia kubadili dini, lakini mimi kama mimi nilikuwa teyari, nilijihisi kumkosa huyu ni kama kupoteza uhai wangu,
Sasa nimeshangaa kusikia baada ya yeye kuniacha, wazazi wangu waliniita kijijini kwetu, nikakaa huko miezi miitatu, siku moja akanitumia sms kuwa nimlete mwanae,(anamtaka) nikaona afadhali, ndio njia ya mimi kurudi kwake, nilikubali na kuja tena dar, wazazi waliniambia nisifikie kwakwe niende kwa ant yangu , alinifata huko na kusema anamtaka mwanae ampleke mwanae machame (akalelewe na wazazi wake) pia bila aibu wala uoga, akatuambia anataka kuoa., hata ant yangu hakuwa akijua hili,
kumuuliza sana akasema anamuoa best friend wangu, na harusi ni mwezi wa kumi kati kati, vikao vimeshaanza. Mwenzenu natamani nijiuwe kabisa, najiona nina mkosi sana, kwanini rafiki yangu anifanyie hivyo? Kwanini itokee kwangu? Kwanini mimi tu? Amechachamaa anamtaka mwanae, sasa mimi nitabaki na nini? Kuna siku nilishika vidonge nimeze nife tu! But nikamuangalia baby wangu alikuwa amelala, nilimuhurumia sana nikaacha, but mawazo ya kujiua bado yananiandama sana jamani nisaidieni, naweza kuivuruga ndoa yao? Lakini kwa haki ipi niliyo nayo? Msaada wenu tafadhali siwezi kula wala kufanya chochote,
nina hali ngumu sana kichwani kwangu