Monday, October 31, 2011

NIMEKUTA SMS YA UTATA TOKA KWA MR. WANGU KUJA KWA HOUSEGIRL WANGU

Nimekuta sms ambayo imetumwa na mume wangu kwa bint wa kazi, sms hii imenipa wakati mgumu sana, yani hata sijui nifanyaje
Wiki iliyopita nilikuwa nyumbani, sikwenda ofisin, kwakuwa nilikua naumwa , basi ilipofika mida ya mchana nilimtuma bint wa kazi aende akanichukulie matunda ya juice sokoni, sasa sijui ilikuwaje akasahau simu yake, nikajikuta nashawishika kusoma sms zake maana simu huwa inamkeep busy sana, na huwa hataki mtu aiguse kabisa, sometimes akipigiwa simu anakimbia kwenda kupokelea nje kabisa na yuko radhi  hata aende na simu bafuni kuoga nayo,  

Sasa siku alipoisahau nikasema hapa hapa, ngoja nione kwanin huwa anaificha sana,  nimejuta jamani, nimekuta mume wangu ametuma sms  inasema hivi (leo umeandaa nini dear ??) na sms inaonyesha imetumwa masaa mawili  yaliyopita,

Ninachojiuliza, mr anajua kabisa kama mimi niko nyumbani, kwanini asinitumie mimi kumuuliza housegirl anaandaa nini? Mbaya zaidi kwanini amuite dear?? Nilipomuuliza  dada baada ya kurudi kwanini baba anakuuliza hivi, akasema sijui mwenyewe, mbona kila siku ananiuliza namuandalia nini?

Nikamuuliza anamaanisha nini anapokuuliza hivi, akasema sijui mwenyewe, (lakini hata jinsi anavyojibu, ni kwa kiburi sana, as if ana jelous na mimi,) nikapiga kwa mr. nikamuuliza kwanini usiniulize mimi, unamuuliza house gil kwan yy ndie mke, mimi si ndio nafanya kila kitu

Akanijibu kuwa napenda kujipa presha za bure kisha akakta simu, nikipiga hapokei, jioni karudi kauchuna hadi sasa hatuongei,

 mwaka umepita  sasa, alishawahi kutembea  na mschana wa kazi ambae nilimfukuzaga baada ya bint kukiri kuwa  kweli ametembea nae,  sasa nahofia na kwahuyu isije kuwa hivyo, nishaurini mwenzen



Monday, October 24, 2011

KABLA HATA SIJAMUOA AMESHAANZA KUSEMA UONGO, (AMESINGIZIA MAMA YAKE KAFA,) NIKIMUOA TUTAWEZANA KWELI??

Habari ya kazi dada, najua Mungu ameweka watu kama nyie ili mwasaidie wale wasiojua, naomba unisaidie dada angu, mimi ni kijana mwenye umri kuoa sasa, mwaka huu mwanzoni nilimpata mdada mmoja ambaye tunapendana sana na nilitaka kumuoa kabisa

Tatizo lilipoanzia ni kwamba, kuna siku alaniambia ana mimba na anaomba kuitoa mimi nikamwomba asitoe kwakuwa nilimuhakikishia kumuoa ina maana mtoto angekuwa kwenye uangalizi mzuri, akanielewa,

baada ya muda mfupi kupita  yeye akarudi kazini kwake alikuwa anafundisha, huku akisoma chuo akiwa chuon kwao siku moja akanipigia simu, akaniambia anaomba nimkopeshe rafiki yake laki mbili ana shida nazo, nikamwambia sina, mambo ni mengi sana, nikahisi amenielewa

kesho yake mchana akabeep nikampigia akapokea mvulana mmoja akasema wewe nani, na mimi nikamjibu mwenye simu yuko wapi, akaniambia mwenye simu ameanguka gafla, na wenzake wamempeleka hospitali, nikaamua  kumpigia rafiki yake nae akawa kama amepaniki akaniambia kuwa yeye(mchumba wangu) ameanguka gafla, kwa kuwa kuna mtu amemjulisha kuwa mama yake amefariki, na aliangukia tumbo mimba imetoka,

kesho yake nikaenda nyumbani kwao (msibani) bila yeye kujua nikamkuta mama yake mzima kabisa, hapo nikajua nimedanganywa, na iliniuma na kunishangaza sana.

toka pale niliamua kukata mawasiliano nae na nilimwambia kabisa kuwa simtaki tena, maana ni muongo, alilia sana na kutubu, niliamua kumsamehe, USIKU ulipofika nikamtomasa akanipa penzi ila nilimwuliza anaweza? akasema ndio,

sasa mimi ni mwanaume naomba niwaulize dada zangu jamani,  mtu akitoa mimba anaweza kufanya mapenzi baada ya siku nne? Na je huyu atafaa kuwa mke wangu kweli??? Maana ameshanistua.



Tuesday, October 18, 2011

NAHIS MAMA NILIYE NAE SI MAMA YANGU MZAZI, NIKIMUULIZA JUU YA HILI NI MKALI SANA NAOMBENI USHAURI WENU

Pole dada violet kwa ujumbe mrefu, hapa nimeufupisha sana
Mimi ni mschana wa miaka 21, akili timamu ya kutambua vitu ilinikuta nikiwa nalelewa na mama tu! Kwa kuwa baba yangu alifariki, 

kwa huyu mama tuko watatu mimi nikiwa mtoto wa kwanza, kwa kuangalia ni kweli tuko tofauti sana sura, maumbile na hata rangi, wao ni weusiii na mimi ni mweupe sana, ila hiyo sio tabu maana baba yangu pia ni mweupe sana, nahisi kuna kitu nyumba ya panzi kimejificha dada v

Huyu mama hapendi maendeleo yangu, yeye pamoja na watoto wake, hadi kufikia kusema hivi ni mengi nimekutana nayo nikiwa chini ya malezi yake, amekwamisha mambo yangu mengi sana, nikimuuliza kuhusu ndugu shangazi zangu upande wa baba anasema baba yangu hana ndugu eti alizaliwa peke yake na wazazi wake (bibi na babu) walishakufa hivyo ukoo nao ulikufa. 
 
Ilitakiwa niende Nje kusoma zaidi, kuna msamalia mwema alijitolea kunisomesha na gharama zote ni juu yake, lakini mama akabana ile nafasi kaenda mdogo wangu wa pili,(mtoto wake), na  bado haikutosha, hataki mimi nifanikiwe na chochote, kuna siku nilimuuliza hivi kweli wewe ni mama yangu? huwezi amini hata kutoka huwa anatoka na huyu mdogo wangu mdogo aliebaki mimi ni kama mschana wa kazi
, naumia sana, naandika huku mahcozi yananitoka dada, kila ninachomwambia anakuwa mkali, na ninapozidi kumuuliza maswali mengi ananichukia sana

Kuna siku alikuja mama mdogo (mdogo wake yeye) na kukuta mama amenipiga hadi mkoo umevimba, nikawasikia wakiongea seblen, mama mdogo akimsema, na kumwambia, au kwavile sio mtoto wako? Hapo ndipo nilipozinguka fahamu kuwa mimi si mwanae kutokana na hivi anavyofanya,

Nisaidieni dada v, nataka kujua ukweli juu ya wazazi wangu, hata kama wote walikufa basi nijuie tu! Hata walipolala, kwanini nanyanyaswa hivi?? Niliwahi kujaribu kumuuliza kidogo tu! Ilikuwa kesi, niliitiwa hadi mjumbe, lakini moyo wangu bado una kitu! HUYU SI, MAMA YANGU.  Nataka kuprove hilo kwanza, nisaidien mdogo wenu, nina wakati mgumu sana
asante dada Violet, 




Monday, October 10, 2011

HOUSEGIRL WANGU ANA UKIMWI, NIMRUDISHE KWAO?AU NIENDELEE KUWA NAE

Mimi ni mama wa mtoto mmoja mwenye umri wa miaka 3, nina mume wangu na tunaishi nyumbani kwao, bado tunajiandaa tuhamie kwetu, tumeamua kuishi  kwa wakwe kutokana na mume wangu kuwa na uhamisho mara kwa mara kutokana na kazi zake

Mimi nina duka langu la nguo Ilala, hivyo kwakuwa huwa nashinda huko ililazimu kutafuta mtu wa kunisaidia kulea mtoto, nilitafutiwa na mkwe wangu, kusema ukweli nilipomuona siku ya kwanza tu! Nilihisi kitu, kutokana na ngozi yake kuwa tofauti na mabakamabaka mengi sana, nikamdadisi sana , akasema huwa ana ugonjwa wa ngozi,

Nilikaa nae wiki moja tu! Nikaamua kumpeleka hsptl bila mkwe wangu kujua, nikamwambia naenda kumtafutia dawa ya ngoz, lakini tulipofika nilimuomba daktar ampime na ukimwi, alipima na kukutwa ameathirka,

Ilinipa wakati mgumu kumueleza, na ikabidi kumwambia mkwe wangu, alisikitika sana,alipomwambia huyu bint cha ajabu wala hakuonyesha hata kustuka, nikamuuliza ulikuwa unajijua kama umeathirika?? Akasema hapana, ila mimi nahisi amenidanganya. 

Lakini pia mama mkwe ananilazimisha niendelee kuwa nae eti thawabu nitapewa na Mungu, mimi binafs sihitaji kuendelea nae, siku niliyomwambia mama amrudishe hadi kwao akawaweke wazi wazazi wake, alikataa na kuniambia ameshamwambia mume wangu kuhusu hilo na mume wangu amekubali huyo binti aendelee kuwepo, kitu ambacho hata sielewi inakuwajekuwaje

Hadi hiv ninavyoandika mimi na mama hatuna mahusiano mazuri kwa ajili ya huyu bint, , na mwanangu nambeba naenda nae dukani kwangu, ninapoondoka na  mtoto mama anasema eti namnyanyapaa huyu binti nifanyaje jamani???


 

Monday, October 3, 2011

KILA NIKILALA, NAOTA NINAMUUA MUME WANGU,








Habari ya kazi dada v, pole, 
mimi nina shida moja ambayo inanisumbua kwa kipindi kirefu sasa, kila nikilala huwa naota nimemuua mume wangu, yani nakuja kushtuka pale aliponyooka na kukata roho, ndio huwa napiga kelele sana na kuamka, nikiamka hujikuta mwili wote unatetemeka, jasho jingi linanitoka, 
mume wangu huniuliza tatizo ni nini? naogopa kumwambia nilichoota, hivyo humdanganya ndogo ingine tu!, huwa anainuka anipa maji ya kunywa kisha nalala, 
imejirudia takriban mwezi sasa, hadi nakosa hata amani, ukizingatia wala sijagombana na mume wangu na wala hata simuwazii kufa, 

yeye mume wangu alinishauri niwe naweka bible kichwani, nalaria, lakini hali hii wala haistop, na mida ya ile ndogo iko pale pale, sasa huwa naweka alarm kwenye simu ikifika mida ile tu! nainuka na kuanza kusikiliza radio, kipindi cha maombi, lakini hujikuta nimepitiwa na usingizi mzito, na nikija kustuka tu! najikuta nimeshaota, na jasho linanitoka,

nampenda mume wangu, naombeni ushauri wenu jamani, pole dada vai kwa kukusumbua, ila naomba usilitaje jina langu, wala email yangu