Tuesday, January 24, 2012

X- BOY FRIEND WA RAFIKI YANGU, ANATAKA KUNIOA, NIKUBALI??


Naomba ushauri dada,
Kuna shemeji yangu (x-boyfriend wa rafik yangu) anataka kunioa, waliachana na rafiki yangu miaka sita iliyopita, kipindi wako wapenzi nilijaribu sana kuwapatanisha, lakini rafik yangu alikataa,baada ya muda rafiki yangu aliniambia kuwa ana boyfriend mpya, sasa mazowea ya mimi na shemeji yangu yamebadilika, badala yake ananipenda mimi, na anataka kunioa kutokana na tabia zangu kuwa nzuri, dada Violet, najikuta namimi naanza kumpenda, nilimwambia rafik yangu, kuwa x wako anataka anioe, akasema niwe na amani tu! Yeye hana neno,
Sasa nishauri dada vai, nikubali?? Maana na mie ninataka kuolewa na nimempenda, nina miaka 26, mwili wangu unahitaji kuwa na mtu, na nimempenda kweli huyu aliyekuwa shemeji yangu, nisaidie dada kunishaur



Friday, January 20, 2012

KITCHEN PARTY GALA



HAYA WALE WADADA/WAMAMA,  MAFUNDISHO KUHUSU NDOA, MAHUSIANO NA VINGINE VINGI  KUTOKA KWA WAZOEFU YAMEFIKA,

 NI KITCHEN PART GALA, ITAFANYIKA KAMA IFUATAVYO
UKUMBI WA DANKEN HOUSE UPO MIKOCHENI KWA WARIOBA BARABARANI KABISA KARIBU NA MBALAMWEZI BEACH.NI UKUMBI MPYA NA WAKISASA.

UMRI NI KUANZIA MIAKA 18 NA KUENDELEA, VAZI LOLOTE LILE WAWEZA VAA MRADI UPENDEZE TU!

KIINGILIO NI TSH 30,000 KWA MTU MMOJA NA KAMA UNAHITAJI MEZA WEWE NA WATU WAKO WA KARIBU NI TSH 300,000
(meza ya watu 10)

MUDA KUANZIA SAA 8 MCHANA MPAKA SAA 2 USIKU

CHAKULA NA VINYWAJI VITATOLEWA

WAZUNGUMZAJI
AUNTY SADAKA

MAMA VICTOR
BI CHAU

Contact to 0789333537

BURUDANI
NYOTA WAZIRI
 (from zeze)


Sunday, January 15, 2012

MUME WANGU HATAKI NIFANYE KAZI YEYOTE


Mume wangu hataki ni fanye kazi, wala baishara yeyote ile,  ananihudumia kweli, lakini mimi sipendi kuwa tegemez, napenda nifatute pesa kwa jasho langu,

Yeye anataka niwe mtu wa ndani tu! Yani hataki niajiliwe wala nijiajiri, anahudumia hadi familia yangu, chochote ntakachosema napewa, lakini nawaza siku tukiachana, kwa namna yeyote ile, iwe by divorce of death, how could I leave ??? si nitapata tabu jamani