Monday, May 16, 2011

KIMAMA ZAIDI,

umeona Unywele huo
 kimama zaidi




Friday, May 6, 2011

ANATAKA TUFANYE MAPENZI KINYUME NA MAUMBILE, NIKIMNYIMA ANACHUKIA SANA, NAMI NAMPENDA NIFANYAJE???

Dada violet, na dada zangu wengine, naombeni mnisaidie mdogo wenu, nilikuwa na mchumba wangu ambae teyari ameshanitolea mahali, kipindi cha mwanzo alikuwa hana tabia ya kunifanya kinyume na maumbile,  yani hajawahi kabisa kuniambia ananitamani huku nyuma,

Lakini hivi karibuni kila tukikutana nae, anataka anifanye, siku ya kwanza alinifanya kwa nguvu, kusema kweli niliumia sana, yani nilimia dada violet, alipomaliza alinishukuru sana, na kesho yake akanipa na zawadi, (ni kama ananibembeleza) nilimfokea sana, na alikuwa kimya,

Mwezi wa tatu, akataka tena kunifanya kwa nguvu, nikamkatalia nikavaa nguo zangu nikaondoka kwake,  tukanyamaziana kama mwezi mmoja, badae akaniomba msamaha nikamsamehe kwakuwa nampenda sana dada, na nikajua keshajirekebisha, baada ya kupatana tukaenda kufanya tena, akalazimisha huku kanibana mikono kwa nguvu, akaipitisha, niliumia sana, yeye alipomaliza akatoa, akaanza kutubu upya,

Nililia sana, sasa ndio kwanza tunataka kuanza vikao vya harusi, kwa style hii nitaweza kweli dada? Wadau naombeni msaada wenu




Monday, May 2, 2011

ALINIDHARIRISHA SANA- SASA ANATAKA TURUDIANE, ANANIFAA KWELI????

Mimi ni mdada ambae sijaolewa, ila nina mpenzi wangu ambae tunapendana sana, yeye kwa sasa hana kazi, mimi ndio huwa namsaidia akiniomba msaada wa hela nampa, cha ajabu dada yangu, ilikuwa jmosi moja alikuwa anakunywa na rafiki zake, akaniita niende, nilikuwa nimebanwa na kazi lakini nilijitahidi nikaenda,

Baada ya kumaliza akaniambia tukaenda hadi kwao kwanza. akasema lazima nilale nae, nikamwambia haitawezekana maana nilikuwa tight sana, alikataa, nikataka kuondoka kwa nguvu, kinachonishangaza akabadilika gafla na kuanza kuongea kwa sauti, " umekula hela yangu nilipe nilipe, nikamuuliza Tshs ngapi?, akasema elfu 20,000, nikaona hali inakuwa mbaya maana alikuwa anaongea kwa sauti kiasi kwamba watu wakaanza kukusanyika, ikabidi nitoe 20,000 nikampa, wakati sijala pesa yake yeye ndioa anakula za kwangu,

akasema bado ingine, na kama simpi nimuachie simu yangu yenye thamani ya 250,000, akaanza kuropoka mbele ya wazazi wake, anongea kwa fujo sana, na vitisho  

anasema " leo nakukata panga kama ujatoa hela yangu", Mama yake na Baba  wakasikitika sana alivyokua ananifanyia Kijana wao, mama yake akaniambia niondoke,

 baada ya wiki 1 akanipigia simu akiniomba msamaha, ukweli moyo wangu unawoga nae sana dada. najiuliza ipo siku atanifanyia kama alivyonidhalilisha, Je mtuu huyu ana mapenzi na mimi, kweli?, naomba ushauri wenu Ndugu zangu.

Samahani dada Violet kwa ujumbe mrefu,  Naomba jina langu liwe kapuni, , Kazi njema Dada.





Friday, April 29, 2011

SEND OFF PARTY OF DIANA

Karibu kwenye maisha ya ndoa Diana, Mungu akutangulie na akutee, akayafanye magumu yote kuwa mepesi kwako, ndoa tamu mwaya,
akiwa bado anaendelea kupambwa








baada ya kupambwa
Hair Style yao


Bi Harusi mtarajiwa alinifurahisha sana, ana pozi za ukweli, haogopi camera hata kidogo


Nikiwa na Mtarajiwa baada ya kumpamba, nimechoka balaaa

Kazi inaendelea



Mama yake akifungwa remba
wewe njoo kama ulivyo, tunabandika na kucha pia
miguu hiyo







KAZINI


 Baada ya kazi (SMILE)
wadada wazuri sana hawa, wamenifurahisha mno, hawana hofu hata kidogo













Wednesday, April 27, 2011

RAFIKI WA MUME WANGU ANANITAKA- NA MKEWE NI RAFIKI YANGU SANA- NIMWAMBIE?

nisaidieni jamani,  kuna baba mmoja ni jirani yetu, ni rafiki sana na mume wangu, wanashirikiana mambo mengi sana, na karibu kila weekend huwa wako pamoja, urafiki wao umefanya mimi na mkewe kuwa marafiki wakubwa, mkewe ananipenda sana,
ninachoshangaa Yule baba anakuja kwa speed ya ajabu, sms kibao, zikiingia tu! Huwa nadelete moja kwa moja, nahofia mume wangu asizione, niliwahi muuliza namba yangu kapata wapi, akasema kachukuwa kwenye simu ya mkewe, nilimfokea  sana, na nilimtishia kuwa nitamwambia mkewe, lakini hakomi  na wala haogopi, kusema kweli hadi sa sa mume wangu sijamwambia, maana mh! Patachimbika,
sasa nahofia siku Yule mama kwa bahat mbaya akipekuwa simu ya mumewe na kukuta sms anazonitumia za mapenzi itakuwaje?? Na nikimwambia kwa sasa ili kujikinga na hatari hiyo atachukuliaje,  najiuliza nimwambie mume wangu au mkewe, au niendelee kuwa kimya,
msaaadaaaa please





Saturday, April 9, 2011

MWILI WANGU UNATOA HARUFU KALI SANA , NINANUKA MASAA YOTE, NAOMBENI USHAURI WENU NITUMIE NINI

Mambo Dada, please usirushe email yangu,
Mimi niko hapa dar, nina miaka 25, tatizo langu ni kwamba ninatoa harufu kali sana, mwili wote, jasho langu lina nunuka sana, kwapa, hata sehemu za siri nanuka pia,  hhali hii inaniumiza sana, inanitesa na kuninyima raha, nakosa kujiamini,

Niliwahi kwenda hospitali, wakafanyia check-up, wakasema nikazane usafi tu, ndio maumbile yangu, lakini sasa mbona hali hiizamani haikuwepo??? Ni miaka mitatu sasa tangu niwe hivi, unakuta hadi nikikaa na watu nahisis wananisema mimi ninavyonuka, kwenye pochi yangu hukos perfume au deodorant za aina 4, kila mara niko washroom najipulizia, hali hii ni ngumu, kwa usafi mimi ni msafi sana, sielezi ni nini hiki,
Nilikuwa na mpenzi wangu mmoja hapa hapa dar, tulidumu kwenye mahusiano miezi mitatu tu! Yeye alikuwa ni msafi sana, sasa harufu yangu ika wa inamkera, nakumbuka kuna siku aliniambia bwana nakupenda, ila harufu yako mimi mmm, hapana siwezi kuvumilia,  nililia sana, sometimes hat akitandani alikuwa akijifunika shuka lake,  finally tukaja kuachana,  alinikwepasana, nikipiga sim hapokei, mara nikasikia anataka kuoa,

Please naombeni ushauri wenu jamani, nisaidieni mwanamke mwenzenu nakosa raha kabisa, muda mwingine huwa nalia peke yangu, serious naombeni msaada wenu, maana perfume zimenichosha sasa, nimetumia manukato yote, sasa nona yamenizowea harufu iko pale pale, sometimes huwa nahisi nimerogwa, nikaa na watu nahisi wote wananisema mimi, na wengine niliwahi kuwasikia kabisa wakinitaja na jina langu, inaniuma sana, bora ingeonekana ni ugonjwa niutibu kwa gharama yeyote,

Please dada usirushe email yangu.