Monday, March 26, 2012

SIKUMWAMBIA KUWA NINA MTOTO.. ANATAKA KUNIOA NA YUKO SERIOUS ,NIFANYAJE????


Habari yako dada violet, mimi ni dada wa miaka 25, nina mtoto wa miaka 4 yuko kwa mama Mtwara, hapa dar naishi peke yangu, sasa niilpata boyfriend .. tulipenda sana, lakini siku moja tukiwa katika maongezi yetu aliwahi kugusia kuwa akitaka kuoa anataka kuoa mtu asie na mtoto wakaanzishe familia yao  peke yao,,,
 niliogopa na kupata hofu ya kumwambia kuwa nina mtoto, mapenzi yaka grow sana na sasa anataka kwenda kujitambulisha nyumbani.. sasa nikimwambia nina mtoto si ataniacha??? Nifanyaje ili anielewe, uhusiano wetu una miaka 2 sasa, na always huwa anapenda kuinsist hicho kitu... najilaumu nafsi yangu kwa kutokuwa wazi from the begining... ushauri wenu please








Thursday, March 1, 2012

NAHITAJI KUOLEWA SASA- ILA SIPATI WACHUMBA WALIO SERIOUS KUOA,


Habari dada Violeth,mimi ni mpenzi wa blog yako,niliona ukitaka kumshauri yule dada ambaye hajaolewa akiwa na miaka 32.Nami nimeona si vibaya nikiomba ushauri kwako.Mimi ni binti ninaekaribia miaka 30,

ninapata wanaume lakini malengo yao yanakua sio mazuri,kiukweli nimechoka kua single natamani kuolewa lakini bado sijapata mwanaume wa kunioa.Sasa nimeanza kwenda kwenye mikesha na kuhudhuria semina mbalimbali za kiroho.
Mbali na kufanya hivyo je ni kitu gani kingine napaswa kufanya? Hope kusikia toka kwako.