Friday, December 31, 2010

I WISH YOU A HAPPY NEW YEAR 2011


Nawatakia wapenzi wangu wooote, heri ya mwaka mpya, Mungu  atulinde, atukumbatie, atubariki kila iitwapo leo, tukumbuke kumshukuru Mungu kwa yoote, hasa uzima tulionao, ukiangalia ni watu wengi sana walitamani na walipanga malengo meengi wayafanye mwaka 2010, lakini wamekufa, hawapo tena, 
tujiulize, sisi ni akina nani mbele za Mungu? tumempa nini Mungu hadi kutufikisha mwaka 2011??? hakuna tulichofanya isipokuwa ni kwa neema yake tu!

Tusianze mwaka tukiwa na vinyonyongo myoni mwetu juu ya maadui zetu, bali tuanze mwaka tukiwa na furaha na wooote, tusameheane tulipokosea na tulipokosewa pia,   tusihesabu makosa, tusiyaweke moyoni, tuachilie roho zetu ziwe nyepesi,  ili Mungu apate nafasi ya kutubariki, we are the Human being, kukosea/kukosewa ni kawaida kwa binadamu, haijalishi umeumzwa kiasi gani, haijalishi umeaibishwa kiasi gani, nafaham shida inakuja pale tunapojaribu kutafakari kile ulichokosewa, ambapo hata kama ni kidogo basi litakuwa kuuubwaaaaaa, NO. tusifanye hivyo, maana kisasi ni juu ya bwana.tusahau yooote yaliyotokea na tuanze mwaka mpya na MUNGU,

MUNGU AWABARIKI WOOOOTE, NA TUSHEREHEKEE MWAKA MPYA KWA FURAHA 
BYE 2010, & WELCOME 2011
NAWAPENDA SANA!!!!!!



Monday, December 27, 2010

MUME WANGU ANAKUNYWA POMBE HADI ANAJINYEA - NIMFANYAJE APUNGUZE AU AACHE KABISA???

Wadau nisaidieni, nimechoka maisha haya,
Mume wangu ni  ni mywaji mzuri sana wa pombe, nilimjua akiwa anakunywa hivyo kumbadilisha ilikuwa ngumu, lakini sasa hivi too much, anakunywa hadi anajinyea, wenzake wanamrudisha hoi, nimemsema mpaka nimekata tamaa, hivi atabadilika kweli?
Nimfanyaje aache pombe, maana hakuna siku anayolala bila kunywa pombe yani bora akose chai kuliko kukosa pombe, kwenye gari huwezi kukosa pombe, hadi jasho analotoa linanuka, akiingia chooni akitoka kila mtu hujua kaingia nani, siku zinavyokwenda anazidi kuchakaa,  namuonea hadi kinyaaa, kuna uwezekano wa kuacha pombe kweli?



Wednesday, December 22, 2010

MERY X MASS & HAPPY NEW YEAR TO ALL

 JALIA,  Says........
What a lovely x-mass  !!!!!!!!!!!!
love you all!!!!! mwaaaaaaaaaaaaaaaa




 JONENSIA Says,
I wish you mary x mass, and  wonderful new year,
Mungu ni mwaminifu kwao wamuombao, nami ni miongoni mwao, na nathibitisha kuwa amekuwa mwaminifu kwangu, nawapenda wooooote, tufurahie kwa furaha na ushindi tele


Jonensia & Eunice
WE LOVE YOUUUUUUUUUUUU

Monday, December 20, 2010

(NAKARIBISHA SALAMU ZA X-MASS NA MWAKA MPYA)


kama wapenda kutuma salamu za x-mass na mwaka mpya, tuma picha kupitia email yangu ambayo ni  violet.gerald@yahoo.com, nami bila hiyana nitakupaisha '' itanoga zaidi kama utatuma na ujumbe wako wa mwaka! ili ninapoipaisha picha yako naambatanisha na ujumbe wako,
 '' mshukuru Mungu kwa kukufikisha mwaka mwingine tena, muombe rehema zake, muombe akuwezeshe kukamilisha malengo yako mema yote uliyoshindwa kufanikisha 2010 ili 2011 yakamilike,
PEKE YETU HATUWEZI- TUNAHITATAJI  SANA MSAADA WA MUNGU!!
KARIBU


 
TYMON AND HIS FRIEND


&  TRACE WITH HER FRIEND


 ARE WISHING YOU A MARY X-MASS &
HAPPY NEW YEAR (2011)


2010  Umekuwa mwaka mwema sana kwa Familia yangu, (mume wangu, na watoto wangu), hadi tunapokaribia kuumaliza mwaka huu,  Namshukuru Mungu kwa kutupa uzima, na baraka zake tele alizoziachilia kwetu. na kutuweka pamoja hadi leo hii kama familia, Im feeling so proud with my  Lovely ''TWINS'', they make me happy always, may the blesses of the Lord be with them for the  all coming years.
WE  LOVE YOU ALL!!!





Wednesday, December 15, 2010

MKE WANGU HAPENDI NDUGU ZANGU HATA KIDOGO- NITAMFANYAJE AACHE TABIA HII


Wanawake wengine sijui wakoje jamani, inahusu nini kuchukia ndugu wa mumeo bila sababu ya msingi, au hata kama kuna hizo ''sababu  za msingi'' watu hukaa na kuongea mkayamaliza, sasa wewe unanuna hata kutembelewa hutembelewi lo! vibaya jamani, wanawake wa tabia hii mjirekebishe, raha kupendwa na ndugu wa pande zote, kupenda kuwa kivyakovyako ni dalili za uchoyo na ubinafsi wala haifai, kaka huyu amenisikitisha kweli,  soma hiyo!!!!!!!!
Nahitaji ushauri wenu sana,
Nilioa miaka miwili katika ndoa yangu, na sikugundua kama mke wangu anatabia hii, maana tulikuwa mbalimbali, tulipojuana tu! Yeye alikwenda South Africa kusoma, namimi nilikwenda UK, baada ya kumaliza, tulikutana Dar, (ambako ndio kwenye familia zetu) tukaanza maandalizi ya ndoa, na hatimae kuona, sikuweza kumchunguza tabia zake, nadhani nilifunikwa na upendo niliokuwa nao kwake.

Shida ni kwamba, mke huyu amechange  kiasi kwamba namuogopa hata mimi, ni mtu wa hasira sana, mtu wa kususa, some times anasusa hata kupanda gari yangu mimi, yuko radhi akapande daladala, sasa mimi maisha haya sijayazowea.

 Ndugu zangu wakija ni mkorofi, anaona kama anabanwa vile, wakati nina nyumba kubwa tu! Na ina nafasi, tena asilimia ya ndugu zangu wako busy na shughuri na familia zao, ila ikifika kipindi cha December wengi hupenda kuja kwangu, kubadilisha mazingira, yani wakifika mke wangu, anachelewa kurudi kwa makusudi tu! Na anaweza kuamka na kutoka bila hata kumsalimia mama yangu na ndugu zangu, yaweza pita hata siku tatu hajawaona.

Mama ni mtu mzima, aligundua hali hii, na akasema kuwa yeye atakuwa haji, ila akinimiss itabidi niwe naenda hata weekend kumsalimia, mama ananipenda sana, maana mimi ni mtoto wa kiume pekee kwa mama yangu,  nikisaidia kwetu nikimwambia tu kwamba nimetuma hela nyumbani, anaweza nuna hata siku nne, bila kusema na mimi, sometimes huwa natuma bila yeye kujuwa.
Nashangaa ndugu zake yeye hawaishi pale kwangu, leo atakuja huyu atakwambia ni mtoto  wa uncle yuko uingereza, kesho atakuja huyu atakwambia ni mtoto wa binamu, mimi huwa sijali 
 maana huwa naamini  wageni  wanaongeza riziki katika familia.

Sasa ndugu zangu wamesusa kuja kwangu, nami nilishazowea wageni, tuna mtoto mmoja tu, ana mwaka na miezi minne, cha ajabu hata ndugu zangu walioko Dar, wakitaka kuja kumchukuwa wakashinde nao kwao mke wangu huwakatalia na husingizia anaumwa.

Naumia sana, naombeni ushauri wenu, naogopa hata kuwaambia wazazi wake maana najuwa baada ya kumsema, nitanyamaziwa hata miezi, na mimi hali hii siipendi na wala sijaizowea, maana hadi huwa naogopa kuwahi kurudi nyumbani siku ambazo amekasirika, mtoto atapigwa na kufokewa kama mtu mzima, naweza kumtandika makofi, lakini nampenda ila nachukiwa tu! tabia zake? je anaweza kubadilika kweli???




Sunday, December 5, 2010

TULIACHANA NA MUME WANGU, AMENINYANG'ANYA WATOTO NA HATAKI HATA NIONGEE NAO-NISAIDIENI


Hello dada yangu violet,
nahitahiji ushauri wako na wadau pia, mimi niliolewa na mume ambae sikumpenda in 2001 and I was 17 years old, ila nililazimishwa na wazazi. Tukafunga ndoa, ndugu zake hawakufika sababu walikuwa hawanipendi, sikujali sana sababu yeye aliiahidi familia yangu ya kwamba atanilinda

tuzaa watoto 3, ila mda ulivyokwenda nae alianza kubadilika, akaanza kunipiga, anarudi usiku sana, Siku zingine harudi kabisa, ilibidi nimshirikishe sheikh mkuu matatizo yetu,  sheikh alimuita lakini hakwenda.

maisha ya ndoa yalinishinda, nikaamua kurudi kwetu mwaka 2008, alininyima talaka, niliamua kuondoka kwa lazima pamoja na wanangu, alhamdulillah nilipata kazi nzuri nawasomesha vizuri

Baada ya muda nikapata safari kwenda UK ndipo nilipo hadi sasa,  watoto nikawaacha nyumbani kwetu, sasa yule bwana alienda nyumbani akawachukua watoto 2. Na toka awachukue, amekata mawasiliano na mimi, hata kuwasiliana na wanangu siwezi.

Nawaombeni wadau na  dada violet mnisaidie, nipeni mbinu zozote, sababu sijui lakufanya kabisa, nimesha tuma watu wakaongee nae aniache niongee  na wanangu, lakini kawakatalia  cha ajabu anasema atawapiga hata hao ndugu zangu  kama wakirudi kwake tena.plz help me sister, I miss my babies so much