Wanawake wengine sijui wakoje jamani, inahusu nini kuchukia ndugu wa mumeo bila sababu ya msingi, au hata kama kuna hizo ''sababu za msingi'' watu hukaa na kuongea mkayamaliza, sasa wewe unanuna hata kutembelewa hutembelewi lo! vibaya jamani, wanawake wa tabia hii mjirekebishe, raha kupendwa na ndugu wa pande zote, kupenda kuwa kivyakovyako ni dalili za uchoyo na ubinafsi wala haifai, kaka huyu amenisikitisha kweli, soma hiyo!!!!!!!!
Nahitaji ushauri wenu sana,
Nilioa miaka miwili katika ndoa yangu, na sikugundua kama mke wangu anatabia hii, maana tulikuwa mbalimbali, tulipojuana tu! Yeye alikwenda South Africa kusoma, namimi nilikwenda UK, baada ya kumaliza, tulikutana Dar, (ambako ndio kwenye familia zetu) tukaanza maandalizi ya ndoa, na hatimae kuona, sikuweza kumchunguza tabia zake, nadhani nilifunikwa na upendo niliokuwa nao kwake.
Shida ni kwamba, mke huyu amechange kiasi kwamba namuogopa hata mimi, ni mtu wa hasira sana, mtu wa kususa, some times anasusa hata kupanda gari yangu mimi, yuko radhi akapande daladala, sasa mimi maisha haya sijayazowea.
Ndugu zangu wakija ni mkorofi, anaona kama anabanwa vile, wakati nina nyumba kubwa tu! Na ina nafasi, tena asilimia ya ndugu zangu wako busy na shughuri na familia zao, ila ikifika kipindi cha December wengi hupenda kuja kwangu, kubadilisha mazingira, yani wakifika mke wangu, anachelewa kurudi kwa makusudi tu! Na anaweza kuamka na kutoka bila hata kumsalimia mama yangu na ndugu zangu, yaweza pita hata siku tatu hajawaona.
Mama ni mtu mzima, aligundua hali hii, na akasema kuwa yeye atakuwa haji, ila akinimiss itabidi niwe naenda hata weekend kumsalimia, mama ananipenda sana, maana mimi ni mtoto wa kiume pekee kwa mama yangu, nikisaidia kwetu nikimwambia tu kwamba nimetuma hela nyumbani, anaweza nuna hata siku nne, bila kusema na mimi, sometimes huwa natuma bila yeye kujuwa.
Nashangaa ndugu zake yeye hawaishi pale kwangu, leo atakuja huyu atakwambia ni mtoto wa uncle yuko uingereza, kesho atakuja huyu atakwambia ni mtoto wa binamu, mimi huwa sijali
maana huwa naamini wageni wanaongeza riziki katika familia.
Sasa ndugu zangu wamesusa kuja kwangu, nami nilishazowea wageni, tuna mtoto mmoja tu, ana mwaka na miezi minne, cha ajabu hata ndugu zangu walioko Dar, wakitaka kuja kumchukuwa wakashinde nao kwao mke wangu huwakatalia na husingizia anaumwa.
Naumia sana, naombeni ushauri wenu, naogopa hata kuwaambia wazazi wake maana najuwa baada ya kumsema, nitanyamaziwa hata miezi, na mimi hali hii siipendi na wala sijaizowea, maana hadi huwa naogopa kuwahi kurudi nyumbani siku ambazo amekasirika, mtoto atapigwa na kufokewa kama mtu mzima, naweza kumtandika makofi, lakini nampenda ila nachukiwa tu! tabia zake? je anaweza kubadilika kweli???