Wednesday, April 28, 2010

MUME WANGU HAJUI KUBEMBELEZA NA HATAKI KUBEMBELEZWA-HATA KITANDANI


Pole na kazi Violet, nimetuma email kama nne hivi, sijaona urushe, ss sielewi ulikuwa huipati au mimi nilikuwa nakosea address?

Tatizo langu ni kwamba mume wangu hajui kubembeleza hata kidogo, yani yeye anafoka masaa yote, na huwa hamalizi jambo, yani analibeba na kulikuza, na atalitumia hilo kukuumiza kila unapokosea,

Hali hii inaninyima raha sana, natamani sana kubembelezwa kama wenzangu, nawatamani sana, yani hata kitandani, utakuta mimi namshika shika, namramba, namchezea sana, lakini yeye anakuwa mgumu utadhani askari aliehisi kuna jambazi pembeni anamvizia, hatikisiki wala kupokea upendo wangu,

Niliwahi kutoka nae na kumueleza ninavyojisikia, akasema tatizo lako wewe nini? Kwani huwa sikufanyi ukaridhika? Mwanzoni hakuwa hivyo, yeye anafanya kazi mimi sifanyi, basi hata ukimpigia simu kama unashida, vile anavyopokea ni kama mligombana, badala ya kusema haloo anasema ehe unasemaje? Sasa ile mimi siipendi kabisa violet, inaniumiza sana

Pia tunapokuwa kitandani, nikitaka kumpa denda, anakuwa kama ananionea kinyaa hivi, nikimnyonya maeneo ya makwapa anakuwa kama ananisukuma hivi wakati hizo ndizo zilikuwa sehemu zake, zamani ukimnyonya sehemu ya kwapa tu! Analegea sana na analia kama mtoto mdogo, violet, situkani wala sitanii, hali hii inaninyima raha, na hata kunipa dozi ni kwa kifupi sana, yani dakika mbili tu amemaliza na hataki kurudia tena, sasa unakuta mmi nakuwa bado nina hamu, naishia kugugumia tu wakati huo yeye anakoroma pembeni, sasa hii si mitego hii? Nikitafuta mwanaume mwingine anikoreze nitakuwa nimekosea? Au nifanyaje?
pia unaweza kuwa unamuelekeza jambo la muhimu na kwa upendo tu! lakini anakuwa kama hakusikilizi, na anaweza fanya hivyo hata mbele za watu, ananitia aibu sana,


Friday, April 23, 2010

NAMNA YA KUWEKA NYUMBA KATIKA HALI YA USAFI







Mara nyingi tumekuwa tunajitahidi kufanya usafi kwenye nyumba zetu. Ila kuna mambo kadhaa huwa tunayafanya kwa uvivu sana ama ni mara chache sana wakati tunasafisha nyumba zetu. Hata maelekezo ya usafi kwa mahousegal/boy huwa hayalengi sana hivi vifatavyo.

1 Hakikisha unatoa nje kapeti la sebuleni unalipiga piga kuondoa vumbi na pia kusafsisha pale sakafuni kwa kuwa pia vumbi hupenye na kutuama chini. Hii ni kwa yale makapeti ya kisasa. Kutofanya hivi kumesababisha kuwa na tatizo la kudumu la kuugua mafua nyumbani bila kujua chanzo na kuona ni kama kawaida tu pale nyumbani.

2 Hakikisha unabadiri mapazia kadiri unavyoweza au kufua mara kwa mara  ili kuondoa mavumbi yanayonasa kutoka nje yarushwayo na upepo. Hii hufanya nyumba kuwa na hewa safi sana. hata kufurahi kukaa chumbani ama sebuleni hata kama ni joto. Si wajua Dar bila joto haijakuwa Dar. hahahahaha

3 Pia kumbuka sana kufuta vumbi lililopo kwenye zile nyavu za kuzuia mbu kwenye dirisha. Tena zile huzuia sana kuingia mbu ndani na hata vumbi, kwahiyo huwa na uchafu mwingi sana unaopunguza hewa safi ndani. Hewa huwa nzito sana na hata kuongeza maumivu ya kichwa. Hapa naweza sema Carbon inatengenezeka. hahaha Bios hiyo.

4 Jambo lingine ni kuhusu viatu, huwa tunavipenda sana viatu vyetu lakini hutchafulia mazingira ya ndani na kuleta taka ndani, bila kusahu harufu mbaya(Vinatema) Inashauriwa viatu viwekwe mahali karibu na mlango wa kutokea au kuingilia. Hii huzuia uchafu kuingia ndani na hata hewa ila mbaya isisumbue ndani na kusababisha makazi kuwa mazito.

5 Hii ni ya mwisho lakini sasa ngumu kiasi hasa kwenye mifumo dume. Kama kaka au baba wa nyumba ni mvuta sigara, aahakikishe ana vuta sigara zake nje kama Mita 15 kutoka eneo la nyumba. Mara nyingi moshi wa sigara hasa utokao mdomoni ndio unamatatizo sana hasa kwa watoto. Yapaswa kushauri wavutaji pale nyumbani watoke nje kwa umbali fulani kisha wamalize hamu zao kisha warudi ndani.


Chanzo cha habari hii ni  lifestyle.msn.com Decor and Organizing.








Wednesday, April 21, 2010

ITAKUWAJE UNAOMBA HOSPITAL FULANI WAKULETEE AMBULANCE

HALAFU WAKATI UNACHUNGULIA DIRISHANI KAMA WAMEFIKA UNAONA KAMA HII....




Kaazi kweli kweli!



DEARS

wapendwa wangu mnaonitumia sms kwamba siirushi mikasa yenu mliyotuma, nataka niwaambie kuwa sijaipata, inawezekana mkawa mmekosea email adress, coz kama mnakumbuka niliwahi kuwaambia kuwa nimebadilisha email adress, so kwa sasa natumia violet.gerald@yahoo.com , kama hamkutumia hii basi mjuwe sijaipata, mbona mikasa mingine naipata fresh tu! kama vipi angalieni vizuri mtakuwa mmekosea email adress.

Tuesday, April 20, 2010

RAFIKI ZANGU WANACHUKULIANA WAUME BILA WAO KUJUA, NIKISEMA NITAKUWA MMBEA?


Kuna kitu kinanichanganya sana, hakinihusu mimi lakini kinawahusu watu muhimu sana kwangu, nina marafiki wawili, na ni wamama wenye familia zao na nimajirani zangu,  ss mmoja kati yako anatembea na mume wa mwenzie wakati wote wawili ni mashoga zangu, ila huyo anaeibiwa hajui kama huyu rafiki yangu mwingine anamchukuwa mumewe, na huwa anamchekea kabisa na kujifanya rafiki yake, wanaongea vizuri sana,

Nilishawahi kumuonya huyu rafiki yangu, kwanza ukizingatia sisi ni majirani, pili huyu akisha kuja kujuwa itaniweka mimi pabaya sana, naona bora hata asingeniweka wazi juu yahili maana linaniumiza sana, kwakuwa huyo mwanaume ameshanogewa na penzi la nje, ameshaanza kujisahau, anamtesa sana mkewe , anampiga sana, anatishia kumfukuza, kitu kidogo tu kwake linakuwa kubwa, huyo dada huwa akipigwa na kufukuzwa anakuja kwangu, akifika kwangu anajieleza sana, na kusema nahisi mume wangu ana mwanamke mwingine,

maana mwanzo hakuwa hivi, anachowaza ni sahihi na mimi nalijuwa hilo, kinachoniuma zaidi sikumoja alipigwa sana mumewe usiku, akakimbilia kwangu, akamkuta na huyu mwizi yuko kwangu, akaanza kutueleza, nilimuhurumia sana, nikamwambia vumilia tu! lakini huy mwenzangu ambae ndie muhusika wa tukio, akawa anamshauri aondoke, aliniudhi sana na huwa namsema sana, lakini hasikii, najuta kwanini nimelijuwa hili, bora ingekuwa siri yao tu!
sasa  kumwambia kuwa chanzo ni fulani,  nashindwa maana wote ni mashoga zangu, Sasa hebu nishaurini, nimwambie tu liwalo na liwe, au nitaitwa mmbea niwaache tu mwenzie huku pembeni anajifanya anampenda, inaninyima raha sana hii.

Thursday, April 15, 2010

PETE ZA NDOA ZINA MAANA GANI KUVALIWA MKONONI?

mh!jamani ni vizuri kwa wajuao wakatuelewesha tusio jua kama mimi, ili nasi tukajua, ni kuhusu pete za ndoa, ambazo now adays zinavaliwa hovyo kama fassion tu!,mtu anavaa as if it was made for decoration,
first time nilikuwa najua pete ya ndoa haitakiwi kuwa na marembo yeyote yale, inatakiwa kuwa plain tu! iwe silver/Gold lazima iwe plain, but i was wrong, coz siku hizi watu wanavaa hata pete za ndoa zenye marembo rembo, na padri anazibariki na watu kuvishana,
yaweza kuwa Gold,

yaweza valiwa silva kama hii, mradi ni pete,

ss pete zinavaliwa kwa ajili ya nini, zina maana au ni pambo la mikononi tu! tena nijuavyo mimi pete ya ndoa ni ya muhimu kuliko hata ya uchumba, maana hata kanisani unapovalishwa pete ya ndoa unatakiwa kuvua hata hiyo ya uchumba uliyoivaa,

hebu tuwekane clear juu ya hili, maswali ambayo huwa najiuliza sana, kama pete ya ndoa ni muhimu mbona wanandoa wengi hawavai? tena sana sana wanaume, hawapendi kabisa kuvaa pete, akitoka kanisani tu! siku ya ndoa basi inawekwa kapuni, hapa ndio ninapo hisi kwamba labda hazina maana
lakini sasa kama hazina maana, kwanini wachungaji kanisani huzibariki, na hata kama ikipotea ukachonga ingine inatakiwa kubarikiwa kwanza? hapo ndipo ninapokuwa confused, hebu tueleweshane juu yahili, ni wengi nakutana nao amevaa pete ya uchumba, au ndoa, unaweza kumpa pongezi , he! umeolewa au unamchumba, hongera, naona pete mkononi, anakwambia ah! ni pambo tu! nasisi tuvaage,
wewe unalionaje hili? 




Tuesday, April 13, 2010

MAMA MKWE ANANIFANYA NITAMANI KUIVUNJA NDOA YANGU- NISAIDIENI

jamani wapendwa wangu, kuna huyu mwenzetu,anahitaji ushauri wetu sana, kusema kweli story yake imenihuzunisha sana, nindefu kidogo, nimejaribu kuiedit kiasi, but tuisome tuilewe ndio tumshauri

Pole na shughuri mdogo wangu, shida yangu ambayo kwakweli nahitaji msaada wenu, ni kwamba, mimi naishi hapa dar es salaam, huku kigamboni, nimeolewa na nina mtoto mmoja wa miaka 3,nilichelewa kuzaa 


Toka nilipoolewa niligundua mama mkwe hanipendi, upande wa mume wangu wamezaliwa wawili tu, yeye na dada yake, ambae anamatatizo ya akili, ana miaka kumi na nne sasa, yani kilema chake hawezi kufanya lolote lile, ni udenda tu unaomtoka masaa yote,
Wakati tunafunga ndoa tulikuwa tumepanga vyumba viwili, mama mkwe wangu akija alikuwa akilala kwenye chumba kingine ambacho nilikifanya kama sebule, anakaa hata miezi mitatu ndio anaondoka, ila ndani ya hiyo miezi mitatu, yani mimi nilikuwa napungua hata mwili, ni mkorofi sana, mwanzoni mume wangu alikuwa upande wangu, alikuwa akinitetea kwa mama, lakini sasa hivi wote wamenigeuka, tangu mume wangu alipokuwa rikizo akaenda kwao, mimi sikwenda kwa ajili ya kazi, basi alikaa mwezi mzima, aliporudi tu! Mambo yakawa mabovu kupitiliza,


Ni kama mtego aliporudi alikuja na huyo dada yake mwenye mtindio wa ubongo, ili niishi nae na kusema maisha ya kijijini na umri wa mama umeenda hawezi kumlea hy bintie , nimeletewa huyo wifi, ni wa kumbeba, hachuchumai kujisadia, wala kupiga mswaki wala nini, akitaka kunya anayaachia tu, mimi nikirudi nafuwa, mahousegilr zaidi ya watano wameondoka wanasema hawawezi kukaa kwa ajili ya ile kero,


Mama mkwe huwa anakuja mara moja moja, na akifika tu! Anaanza vijembe, mara mwanangu ameisha sana, hali vizuri, mambo mengi sana, niliwahi kuongea na mume wangu, nikamwambia huyu jesca kwanini tusimpeleke kule wanakolea watoto wenye hali kama hii? Akakataa, akasema wanapelekwa wasio na ndugu, nimlee tu, na kama sitaweza niondoke mimi. Inaniuma sanahii, na nikiondoka nani atamsadiia


Mume wangu ni muislam, na mimi ni mkristo, kunasiku wote tulikuwa kazini, Yule binti mlemavu wa akili(wifi yangu) alipata kama kifafa vile, akaanguka na kutapatapa, housegirl wangu alikimbia kwenye nyumba ya jirani yetu(mlokole) wakaja kumfanyia maombi, alitulia, niliporudi ndio nikapewa taarifa ile, basi mimi nilimuhadithia mume wangu aliporudi kwania njema tu, violet nilipigwa mimi na housegilr wangu, tulipigwa sana, kesho yake msichana wangu aliondoka kurudi kwao, nikaachwa na mtoto wangu tu! Akaagizwa mama mkwe akaja, waliweka kikao walinisema sana

Nilimwambia mume wangu basi tuwe na wasichana wawili, wa kumlea huyu mdogo wako, na wakumlea mwanangu wote wawili nitawalipa mimi, lakini alikataa nakusema kuwa najifanya nina pesa, ataniachisha kazi, sasa jamani hadi sasa hvi mimi sijui cha kufanya, nilimshauri basi tumpeleke mtoto boding alikataa, sasa niambieni wanandoa wenzangu, nifanye nini? Hamna amani nyumbani, kila siku ugomvi, kipigo, mama mkwe anakazana tu kuwa nina roho mbaya, dini yao inaruhusu mimi kuachwa au kuolewa mke mwenza, na mume wangu anasema kama nimechoka kumuhudumia dada yke basi nikubali aoe mke mwingine wa kumuhudumia jesca, nawaza niondoke na mtoto wangu, au niendelee kukaaa? Au nifanyaje jamani? maana sometimes huwa nahisi kama vile wao ndio walimuharibu akili, kwanini hawataki apate msaada wa maombi





 

Friday, April 9, 2010

LO! SASA JAMANI HUYU DADA ANASHIDA GANI KWANI?

Lo!
nimejaribu kufikiria hii ni sababu ya nini, nimekosa jibu, nimejikuta nacheka sana,
mwenyewe sijui hajijui kama nyumba kumeharibika lo!

Thursday, April 8, 2010

MUME WANGU ANATABIA YAKUTEMBEA NA MAHOUSEGIRL WANGU- JE NIWE NAWAWEKA WAZI JUU YA TABIA YAKE KABLA??

Anayo tabia hiyo, mimi binafsi imeniumieza sana na kunifanya naiona hali ya kawaida tu,

Maana kila anaekuja anaondoka kwa sababu hizo hizo, mwanzoni sikuwa nilikuwa naumisa sana, nikawa naondoka moja kwa moja kwetu, ananifata narudi, kwa ajili ya watoto wangu tu!,

Kuna kipindi alimpa mimba housegirl wangu huyo alikuwa ni watano, nililia sana, maana kuna jirani yangu yeye ni nesi, ndio alieniambia kwamba nimchunguze, mimi kutwa nipo kazini, narudi usiku na watoto wanakuwa wamelala

Yeye huwa anawahi kurudi, basi kumbe ule mchezo wanaufanya kipindi ambacho sipo, basi nilipoanza kumchunguza kweli nikaona maziwa yanamjaa na anapendeza sana, ila kazi anafanya kama kawaida, sema alikuwa ananidharau kupita kiasi, mimi sina tabia ya kuongea ongea, ni mvivu sana kusema sema, lakini ilifika kipindi msichana ndio akawa kama mama,

Siku ya siku ilifika nikambananisha sana, nikiwa na Yule nesi jirani yangu, akampima, akakutwa na mimba, tukaanza kumuuliza ni yanani, alikataa kusema, baada ya kuamua kumfukuza ndio akasema ‘’ ntaenda wapi wakati muhusika ni baba’’ nilitaka kurukwa na akili kabisa

Mume wangu nilipomuuliza mara ya kwanza alikataa, nililia sana, nilipombana sana ndio akakubali na kuniomba msamaha,

Kusema kweli niliamua kurudi kwetu rasmi, nikamuelezea mama hali halisi, mama akaniambia nipumzike nyumbani kwanza, maana matatizo yalikuwa yamefuruliza sana,

Lakini nilipigiwa simu na kuambiwa mwanangu amelazwa, anaumwa sana, maana nikitaka kuondoka na watoto ananikatalia, hivyo niliondoka peke yangu, kwa ajili ya mwanangu nilirudi nikafikia kwa Yule nesi, rafiki yangu, nikawa namuuguza mwanangu, sasa kuna siku alinifata usiku yeye na ndugu zake na kunitaka nirudi nyumbani tukayaongee, niliwaheshimu sana, name nilimpigia simu mama yangu, akaja, tukayaongea huku Yule msichana arudishwe kwao, sasa sielewi, kabla yule msichana hajaondoka, tukiwa katika maandalizi ya kumsafirisha, nahisi kuna mchezo ulifanyika, maana baada ya miezi mitatu, Yule binti mimba ilitoka, akuwa anaumwa, nahisi alikunyw vidonge ili itoke, au mume wangu alimshawishi aitoe, kusema kweli niliamua kumrudisha kwao, mume wangu alisemwa sana na ndugu zake, na akaomba msamaha kutorudia,

Nilipoletewa mwingine tena, akamtongoza, huyu wa sasa alikuwa mwaminifu, akaniambia mama, baba kasema nilale nae atakuwa ananipa mshahara mkubwa na kuwajengea nyumba wazazi wangu, nilimsema sana, nilimuuliza mimi tatizo langu ni nini hadi utake kunifanyia wasichana wangu? Kwanini unanidharirisha hivyo? Hakujibu, isipokuwa alimchukia sana Yule binti, na kuna kipindi nilisafiri kikazi nikakuta amemfukuza nyumbani kamleta mdogo wake,


Sasa nahitaji ushauri wenu, niwe nawaweka wazi wasichana ninaowapata juu ya tabia ya mume wangu? Au nitakuwa namdharirisha? Ila hali hii imenifanya nijishushe thamani sana, kwanini asifanye nje huko? Kuna wazuri wangapi hadi ang’ng’ane na wasichana wangu?





Monday, April 5, 2010

NIMECHANGANYIKIWA- MCHUMBA WANGU ANANING'ANG'ANIA NIMFANYE KINYUME NA MAUMBILE

Nipo Mwanza ni kijana mwenye umri wa miaka 28 nina mchumba ambae yeye ana umri wa miaka 25.uchumba wetu umeanza miaka 3 iliyopita ambapo mpaka sasa hata kwao wananijuwa na nipo katika process za kufunga ndoa na mahari nimetoa, bado ndoa ambayo tulipanga kufanya tarehe 12/06/2010 katika kipindi chote cha uchumba tuliweka ahadi ya kutofanya mapenzi mpaka ndoa.

siku moja mchumba wangu alikuja nilipopanga, kama kawaida mkikaa chemba wawili wa jinsia tofauti, chochote kinaweza tokea. Tulijikuta tunaanza kuchezeana na tukajikuta tumevunja ile ahadi tuliyoweka ila mbaya zaidi mchumba wangu alitaka nimfanye kinyumbe na maumbile " NIMLE TIGO "

hapo ndipo mimi nilipohamaki na kumuliza je mchezo huo ameanza lini na alinijibu kwamba alitaka ajaribuuu kwangu tu.Tabia hiyo ilinichukiza mpaka nikamuwa kuachana nae ila aliniomba msamaha na kuniahahidi kutorudia kunitamkia hilo neno yaani kufanya mapenzi kinyume na maumbile.

Tatizo majuzi tu alikuja home kwangu tulale wote, usiku wakati mimi nimepitiwa na usingizi nilishituka ghafla baada ya kuhisi uume wangu unaguswa guswa, nikaamka, nilimkuta mchumba wangu amejiingiza uume wangu kwenye njia yake haja kubwa kwani mimi nilala chali na yeye ndio aliponikalia kwa matako na kujiingiza uume katika njia yake ya haja kubwa?

Nilishikwa na hasira sana, nikamuuliza kwa hasira, unafanya nini? na yeye alibaki kimya, nilikasirika sana na kuamua kumtimua kwangu usiku na nikamwambia simtaki tena .

Mbaya zaidi huyu binti nishamfanyia mambo kibao kwani nilimkuta hana mbele wala nyuma na mimi ndie niliyemsomesha amefika kidato cha sita na kupata kazi huku akitarajia kuingia chuo mwaka huu na tayari nimetumia ghalama nyingi kwa ajili ya ndoa.je ndugu zangu huyu mtu nimsamehe kama anavyodai yeye, kwamba hatarudia tena, au niendelee na msimamo wangu? Yani nimwache? Kumpenda bado nampenda sana. Nisaidieni ushauri

Friday, April 2, 2010

MUME WANGU NI MCHAFU SANA, ANANITIA HATA KINYAA- NISHAURINI NIFANYE NINI

Nimerudi jamani, mpanaaaaaaaaa, niliwamisi sana, thanks God nimemaliza mitihani yangu salama, nasubiri majibu tu! asante kwa mliokuwa mmenikumbuka, nami niliwakumbuka sana tu! sema mshika mawili moja au yote yaweza mponyoka, ikabidi niache kwanza huku ili nibase kwenye kitu kimoja, now im back to you dears, na nyie miliotuma sms hizi

1. umefulia wewe, huna jipya, story zako tumezichoka, unafikiri kuendesha blog ni kazi ndogo, huwezi
2. huwezi kuendesha blog wewe, unasingizia mitihani, waachie wenyewe, waTZ wote hamjui kuendesha blog, acheni  mnatukera ah!

NAPENDA kuwaambia hivi, nimewasamehe bure kwakuwa hamujui mlitendalo, pia huwa najua kuwa hakuna shamba litakalojaa mazao peke yake, lazima na magugu yawemo, basi watu wa style yenu wala haminipi shida, kuhusu blog za kitz kukukera, kwani umelazimishwa kusoma blog yangu, si usome hizo za nje? blog ziko kibao kwanini msisome hizo?? kuna wanaonufaika kupitia blog yangu, ushauri wa watu umewasaidia, wameweza kupata mwanga wa kutatua matatizo yao, ss kama wewe unaona haukufai, usiwe unaifungua blog yangu, waaachie wale wanaona inawafaa. OVER

(TURUDI KWENYE MKASA WETU WA LEO, NIMEIKUTA MINGI KIMTINDO, LAKINI TUANZE NA HUU KWANZA)]

Violet mambo vipi? mimi nina tatizo moja, na linaninipa shida sana, naomba ushauri wenu,
Nimeolewa, na mwanzoni tulikuwa tunaelewana sana na mume wangu, alikuwa na kazi, lakini baada ya muda akawa hana kazi tena, yeye ni mtu wa kukaa nyumbani tu! anasubiri mwisho wa mwezi nimgawie hela ili akalewee pombe,
shida inakuja hapa, akishalewa tu akirudi hata usiku wa manane anafikia chooni,(chumbani kwangu kuna choo) basi anachokijua yeye ni kuchamba tu! anakunya, mavi anaacha kama yalivyo, hadi ninapofanya usafi asubuhi, ndio nifrash, na hii ni tabia yake, ukimwambia anachofanya ni kosa, anafoka anasema yeye ni kichwa cha familia, hivyo tumsikilize yeye tu!,
shida ingine ni kwamba, yeye ni mtu wakurudi usiku tu, na akirudi ule usiku, anataka nimpe, sasa mimi huwa nasikia kinyaa sana, maana amelewa sana, mwili wote ananuka pombe, halafu anakuwa ananitaka, inanipa wakati mgumu sana, hii tabia ya uchafu wa chooni na hata kusex nae naona kinyaa, pia mume wangu si mtu wa kushaurika, hata umshauri vipi, hashauriki kabisa, sasa violet na wengine, naombeni mniambie nifanyaje mwenzenu, maana loh! inanikera sana mimi.