jamani wapendwa wangu, kuna huyu mwenzetu,anahitaji ushauri wetu sana, kusema kweli story yake imenihuzunisha sana, nindefu kidogo, nimejaribu kuiedit kiasi, but tuisome tuilewe ndio tumshauri
Pole na shughuri mdogo wangu, shida yangu ambayo kwakweli nahitaji msaada wenu, ni kwamba, mimi naishi hapa dar es salaam, huku kigamboni, nimeolewa na nina mtoto mmoja wa miaka 3,nilichelewa kuzaa
Toka nilipoolewa niligundua mama mkwe hanipendi, upande wa mume wangu wamezaliwa wawili tu, yeye na dada yake, ambae anamatatizo ya akili, ana miaka kumi na nne sasa, yani kilema chake hawezi kufanya lolote lile, ni udenda tu unaomtoka masaa yote,
Wakati tunafunga ndoa tulikuwa tumepanga vyumba viwili, mama mkwe wangu akija alikuwa akilala kwenye chumba kingine ambacho nilikifanya kama sebule, anakaa hata miezi mitatu ndio anaondoka, ila ndani ya hiyo miezi mitatu, yani mimi nilikuwa napungua hata mwili, ni mkorofi sana, mwanzoni mume wangu alikuwa upande wangu, alikuwa akinitetea kwa mama, lakini sasa hivi wote wamenigeuka, tangu mume wangu alipokuwa rikizo akaenda kwao, mimi sikwenda kwa ajili ya kazi, basi alikaa mwezi mzima, aliporudi tu! Mambo yakawa mabovu kupitiliza,
Ni kama mtego aliporudi alikuja na huyo dada yake mwenye mtindio wa ubongo, ili niishi nae na kusema maisha ya kijijini na umri wa mama umeenda hawezi kumlea hy bintie , nimeletewa huyo wifi, ni wa kumbeba, hachuchumai kujisadia, wala kupiga mswaki wala nini, akitaka kunya anayaachia tu, mimi nikirudi nafuwa, mahousegilr zaidi ya watano wameondoka wanasema hawawezi kukaa kwa ajili ya ile kero,
Mama mkwe huwa anakuja mara moja moja, na akifika tu! Anaanza vijembe, mara mwanangu ameisha sana, hali vizuri, mambo mengi sana, niliwahi kuongea na mume wangu, nikamwambia huyu jesca kwanini tusimpeleke kule wanakolea watoto wenye hali kama hii? Akakataa, akasema wanapelekwa wasio na ndugu, nimlee tu, na kama sitaweza niondoke mimi. Inaniuma sanahii, na nikiondoka nani atamsadiia
Mume wangu ni muislam, na mimi ni mkristo, kunasiku wote tulikuwa kazini, Yule binti mlemavu wa akili(wifi yangu) alipata kama kifafa vile, akaanguka na kutapatapa, housegirl wangu alikimbia kwenye nyumba ya jirani yetu(mlokole) wakaja kumfanyia maombi, alitulia, niliporudi ndio nikapewa taarifa ile, basi mimi nilimuhadithia mume wangu aliporudi kwania njema tu, violet nilipigwa mimi na housegilr wangu, tulipigwa sana, kesho yake msichana wangu aliondoka kurudi kwao, nikaachwa na mtoto wangu tu! Akaagizwa mama mkwe akaja, waliweka kikao walinisema sana
Nilimwambia mume wangu basi tuwe na wasichana wawili, wa kumlea huyu mdogo wako, na wakumlea mwanangu wote wawili nitawalipa mimi, lakini alikataa nakusema kuwa najifanya nina pesa, ataniachisha kazi, sasa jamani hadi sasa hvi mimi sijui cha kufanya, nilimshauri basi tumpeleke mtoto boding alikataa, sasa niambieni wanandoa wenzangu, nifanye nini? Hamna amani nyumbani, kila siku ugomvi, kipigo, mama mkwe anakazana tu kuwa nina roho mbaya, dini yao inaruhusu mimi kuachwa au kuolewa mke mwenza, na mume wangu anasema kama nimechoka kumuhudumia dada yke basi nikubali aoe mke mwingine wa kumuhudumia jesca, nawaza niondoke na mtoto wangu, au niendelee kukaaa? Au nifanyaje jamani? maana sometimes huwa nahisi kama vile wao ndio walimuharibu akili, kwanini hawataki apate msaada wa maombi